LIVE STREAM ADS

Header Ads

Majukwaa ya NAWEZA na SITETEREKI kuzinduliwa Kanda ya Ziwa

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Judith Ferdinand, BMG
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imejipanga kuboresha huduma za afya ya uzazi kwa akinamama, watoto chini ya umri wa miaka mitano pamoja na vijana kupita majukwaa ya Naweza na Sitetereki chini ya mradi wa Tulonge Afya unaofadhiliwa na shirika la watu wa Marekani (USAID).

Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Mwanza, Afisa Mradi wa Afya ya Uzazi Salama (MOHCDGEC) kutoka wizara hiyo, Martha Shakinyau alisema majukwaa hayo yanalenga kutoa elimu kwa umma ili kupunguza vifo vya akina mama wakati wa kujifungua kutoka vifo 556 kati ya vizazi hai 100,000 kwa mwaka hadi kufikia 292 ifikapo mwaka 2020.

Alisema pia yamelenga kuwahamasisha akina mama wajawazito kuhudhuria kliniki kwani idadi ya wanaohudhuria klinikini hivi sasa ni asilimia 25 huku malengo yakiwa ni kuongeza idadi hiyo hadi kufikia asilimia 70 mwaka 2020.

Aidha alibainisha kwamba asilimia 63 ya akina mama wajawazito ndio hujifungulia katika Vituo vya Afya ama Hospitalini huku asilimia 34 wakifika kwenye huduma za afya baada ya kujifungua.

“Tumekuja na jukwaa la Naweza ili baba, mama, familia na kila mmojkatika jamii aweze kuwajibika katika kuwashawishi na kuelimisha akinamama wajawazito kwenda kliniki pale wanapogundua kuwa na ujauzito”. Aalisema Shakinyau.

Naye Afia Mradi wa Mawasiliano ya Afya, Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Tumaini Haonga alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa ya kusaidia akinamama na jamii kwa ujumla kupata elimu ya uzazi ili kufikia asilimia 70 ya wajawazito wanaohudhuria kliniki kabla na baada ya kujifungua.

Kwa upande wake Mratibu wa Afya ya Uzazi kwa Vijana kupitia jukwaa la Sitetereki, Gerald Kihwele alisema jukwaa hilo limeanzishwa kwa lengo la kuboresha shughuli za mawasiliano ya mabadiliko ya tabia kwa vijana kuanzia miaka 15 hadi 24 nchini na kuwahamasisha kuwa na tabia za kiafya ambazo zitaboresha hali zao na afya kwa ujumla.

Mkurugenzi  wa Mawasiliano, Mradi USAID Tulonge Afya, Prisca Rwezahura alisema waandishi wa habari wanategemewa katika kuboresha huduma za afya kwa kutoa elimu kwa wananchi ili kubadilika na kulinda afya zao.

Majukwaa ya NAWEZA na SITETEREKI kupitia mradi wa Mradi wa Tulonge Afya yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi Machi 06 na 07, 2019 kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa ambapo uzinduzi huo unafanyika Jijini Mwanza. Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.