LIVE STREAM ADS

Header Ads

Warsha ya utetezi wa Sheria za Vyombo vya Habari yafanyika mkoani Pwani

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Washiriki wa warsha ya utetezi wa Sheria za Vyombo vya Habari iliyoandaliwa na kuendeshwa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afya MISA tawi la Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la kimataifa la Utetezi wa Haki za Kijamii ICNL.

Katika kuendeleza hamasa na kutetea uhuru wa kujieleza katika jamii, MISA Tanzania na shirika la utetezi wa sheria na haki za kijamii la ICNL zimewakutanisha wadau mbali mbali katika warsha ya utetezi wa sheria za vyombo vya habari. Warsha hiyo imehudhuriwa na wadau mbalimbali wa tasnia ya habari,asasi za utetezi wa haki za binadamu, wanasheria pamoja na wahadhiri wa vyuo vikuu.

Warsha hiyo ya siku mbili iliyofanyika mjini Bagamoyo ililenga kuwakutanisha wadau hao kwa lengo la kuzifahamu, kuzielewa na kujadili namna sheria za vyombo vya habari zinavyo athiri mazingira ya kazi za kiuandishi pamoja na uhuru wa kujieleza kuanzia ngazi ya taifa hadi kimataifa.
Kaimu mkurugenzi wa MISA Tanzania, Gasirigwa Sengiyumva akikaribisha washiriki na kutoa neno la ufunguzi katika warsha ya utetezi wa sheria za vyombo vya habari.

Akizungumza wakati wa ufunguzi Kaimu Mkurugenzi wa MISA Tanzania, Gasirigwa Sengiyumva alitoa wito kwa wadau wa masuala ya habari kuendelea kupaza sauti bila kuvunja sheria akisisitiza uhuru wa kujieleza ni haki ya kila mmoja.

Kadhalika akielezea umuhimu wa uwepo wa sheria rafiki katika kufanya mazingira yawe salama kwa tasnia ya habari, Aloys Habimana kutoka shirika la kimataifa la utetezi wa haki za kijamii la ICNL lenye makao makuu yake nchini Marekani alisema changamoto ya sheria zisizo rafiki kwa taaluma ya habari na uhuru wa kujieleza ni changamoto sehemu nyingi duniani Afrika ikiwa na mifano halisi.
Bw.Aloys Habimana kutoka shirika la kimataifa la utetezi wa haki za kijamii la ICNL akiendesha warsha ya utetezi wa sheria za vyombo vya habari iliyoandaliwa na kuendeshwa na MISA kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la utetezi wa haki za kijamii la ICNL.
"Pamoja na mazingira haya nawasihi msivunjike moyo wala kukata tamaa, masuala ya kisheria hayabadiliki kwa siku moja yanahitaji kupitia hatua kadhaa na kila jambo linaweza kupatiwa ufumbuzi hasa wadau wote watakaposhirikiana na kujenga hoja zenye ushawishi na tija kwa pande zote". Alisisitiza Aloys.

Sambamba na hilo, Lily Liu ambaye ni mjumbe kutoka ICNL aliahidi kuwa shirika lao litaendelea kushirikiana na wadau husika katika nyanja zote ili kufanikisha na kutimiza adhma ya kuwa na jamii isiyo na sheria kandamizi zinazoathiri dhana nzima ya uhuru wa kujieleza na vyombo vya habari.
Lily Liu kutoka shirika la kimataifa la utetezi wa haki za kijamii la ICNL akijadili jambo pamoja na wadau walioshiriki warsha hiyo.
Mwandishi mkongwe na mshauri wa masuala ya habari Rose Mwalimu maarufu kama "Mama Rose" akielezea jambo kwa washiriki wenzake.
Washiriki warsha hiyo wakijadili baadhi ya sheria na kanuni katika makundi.
Na Fredy Njenje

No comments:

Powered by Blogger.