LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wasaidizi wa Kisheria Manispaa ya Shinyanga wapigwa msasa

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Jumla ya Wasaidizi wa Kisheria 36 katika Masoko ya Manispaa ya Shinyanga wamepatiwa mafunzo ya Sheria na Shirika la Agape AIDS Control Programme ili wakasaidie kutoa elimu hiyo kwa wafanyabiashara kwa lengo la kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wasichana na wanawake wafanyabiashara masokoni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape, John Myola akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya Sheria ya siku tatu kwa Wasaidizi wa Kisheria Manispaa ya Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape, John Myola akisisitiza jambo kwenye mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape, John Myola akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.
Afisa Masoko Manispaa ya Shinyanga, Alex Hinda akitoa mada kuhusu namna bora ya kufanya biashara na kuwataka wafanyabiashara kujitahidi kutunza taarifa zao za fedha.
Afisa Masoko Manispaa ya Shinyanga, Alex Hinda akitoa mada wakati wa mafunzo hayo.
Wasaidizi wa Kisheria wakiwa ukumbini.
Wasaidizi wa kisheria wakiwa ukumbini.
Wasaidizi wa Kisheria wakifanya mtihani wa kipimo cha uelewa wa mafunzo hayo.
Wasaidizi wa Kisheria wakifanya mtihani.

Wasaidizi wa Kisheria wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mafunzo kufungwa.
Wasaidizi wa Kisheria wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mafunzo kufungwa.


Na Kadama Malunde - Malunde1 Blog
Jumla ya Wasaidizi wa Kisheria 36 katika Masoko ya Manispaa ya Shinyanga wamepatiwa mafunzo ya Sheria na Shirika la Agape AIDS Control Programme ili wakasaidie kutoa elimu hiyo kwa wafanyabiashara kwa lengo la kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wasichana na wanawake wafanyabiashara masokoni.

Mafunzo hayo yaliyodumu kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa Katemi Hoteli Mjini Shinyanga yalihitimishwa Jumapili Machi 31,2019 na Mkurugenzi wa Shirika la Agape, John Myola.

Myola alisema katika mafunzo hayo, Wasaidizi wa Kisheria wamepewa elimu kuhusu sheria mbalimbali na kutambua haki za binadamu, haki za kiuchumi, jinsi ya kufanya biashara, ukatili wa kijinsia na mahali sahihi pa kutoa taarifa za vitendo vya kikatili.

Alisema mafunzo hayo ni mwendelezo wa utekelezaji wa mradi wa "Mpe Riziki Si Matusi" kwa lengo la kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana wafanyabishara katika masoko unaofadhiliwa na Shirika la UN WOMEN kupitia Shirika la kitaifa la Equality for Growth (EfG).

"Naomba mafunzo haya mliyopata yatakuwa msaada kwenu binafsi lakini pia nendeni mkawasaidie wananchi, katoeni huduma bila upendeleo na bila kuonea mtu ili kuhakikisha kila mfanyabiashara anapata haki sokoni". Alisema Myola.

"Nawashauri pia kutunza siri za watu, msiwe waoga kutatua migogoro inayotokea sokoni,naamini mtakuwa mstari wa mbele kupiga vita dhuluma mbalimbali ikiwemo rushwa ya ngono na kuwapigania akina mama na wasichana ambao wana maumivu ya kutendewa vitendo vya kikatili". Aliongeza Myola.

Aliyataja masoko ambako mradi huo unatekelezwa katika Manispaa ya Shinyanga kuwa ni Soko Kuu Mjini Shinyanga, Kambarage, Nguzo Nane, Ibinzamata, Ngokolo Mitumbani na Majengo Mapya.

No comments:

Powered by Blogger.