LIVE STREAM ADS

Header Ads

Zoezi la ukaguzi wa vyoo bora lapamba moto Kaya kwa Kaya wilayani Ilemela

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com


Judith Ferdinand, BMG
Wakazi wilayani Ilemela wamehimizwa kubadili fikra na kuwa na utamaduni wa kujenga vyoo bora na kuvitumia badala ya kusubiri hadi mamlaka za Serikali ziwafikishe kwenye vyombo vya sheria.

Afisa Afya wilayani humo, Petro Joseph ametoa rai hiyo wakati akizungumzia zoezi la ukaguzi wa vyoo bora katika ngazi ya Kaya, lililoanza mwezi Januari mwaka huu ambalo hufanyika kila baada ya miezi mitatu.

“Wananchi wawe na tabia ya kujenga na kutumia vyoo bora, wasisubiri hadi wafikishwe kwenye vyombo vya sheria”. Alisema Joseph.

Alibainisha kwamba Sheria ya Afya ya Jamii namba moja ya Mwaka 2009 inatoa mwongozo wa kuwafikisha mahakamani wananchi wasio na vyoo bora hivyo wananchi wasisubiri hatua hiyo badala yake wawe na vyoo bora hatua itakayosaidia kuoambana na maginjwa ya milipuko.

#PamojaDaimaBMG

No comments:

Powered by Blogger.