MWANZA- Biteko akutana na Wenyeviti wa Bodi zilizo chini ya Wizara ya Madini
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa
Madini, Doto Biteko amekutana na Wenyeviti wa Bodi za taasissi zilizo chini ya
wizara hiyo kupitia kikao kazi kilichofanyika jana Julai 03, 2019 jijini
Mwanza.
Kikao hicho
cha kwanza baina ya Waziri Biteko na Wenyeviti hao tangu wateuliwe kwenye
nafasi zao, kililenga kujadiliana namna ya kuboresha utendaji kazi baina ya
taasisi zote bila kuingiliana kimajukumu.
Kando ya
kikao hicho, Waziri Biteko akawaeleza wanahabari kwamba majadiliano hayo yatawasaidia
Wenyeviti hao kuendesha taasisi zao kwa weledi huku Wizara ya Madini ikinufaika
na mchango wao kazini kwani wote wana uzoefu wa kutosha na hivyo kutimiza matarajio
ya watanzania kuona wananufaika na Wizara hiyo.
Waziri
Biteko pia alitumia fursa hiyo kuendelea kuwahimiza wachimbaji na
wafanyabiashara wa madini kuachana na utoroshaji wa madini na badala yake
wayatumie masoko ya madini yaliyoanzishwa katika maeneo mbalimbali nchini kuuzia
madini yao na kwamba wanaokiuka utaratibu wataendelea kushughulikiwa kisheria.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: