LIVE STREAM ADS

Header Ads

Bugando yaboresha matibabu kwa wenye vichwa maji na mgongo wazi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Wazazi na walezi wa watoto wenye matatizo ya vichwa maji na mgongo wazi wamehimizwa kuwafikisha katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa Bugando iliyopo jijini Mwanza kwa ajili ya matibabu badala ya kuwaficha nyumbani wakidhani matatizo hayo yanatokana na imani za kishirikina.

Hayo yalielezwa jana Julai 22, 2019 na Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji katika Hospitali ya Bugando, Dkt. Fabian Massaga baada ya Hospitali hiyo kupokea ugeni kutoka Shirika la “Child-Help International” ambalo limekuwa likifadhili uboreshaji wa matibabu ya vichwa maji na mgongo wazi hospitalini hapo.

Mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake ana tatizo la kichwa kikubwa aliushukru uongozi wa Hospitali ya Bugando kwa kutoa bure huduma ya upasuaji kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi huku akishauri Hospitali hiyo kupunguza gharama za dawa na vipimo ikiwemo “CT-Scan” kwani bado ni changamoto kwao.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.