TANAPA yaeleza fursa za Utalii mikoa ya Kusini, Magharibi na Kaskazini Magharibi
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Kamishna wa Uhifadhi wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Dkt. Allan Kijazi akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa mwaka wa TANAPA, Wahariri na Wanahabari Waandamizi, jana Julai 04, 2019 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akitoa salamu zake kwenye mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi.
Mgeni rasmi, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangala akifungua mkutano huo wa siku mbili kuanzia jana.
Washiriki wa mkutano huo.
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na washiriki wa mkutano huo.
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na washiriki wa mkutano huo wenye lengo la kuimarisha mahusiano baina ya TANAPA na vyombo vya habari katika kuhamasish Utalii na Uhifadhi Tanzania.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwala alipowasili ofisini kwake.
#BMGHabari
Mamlaka ya
Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imebainisha kuelekeza nguvu zaidi katika kutangaza
fursa za utalii zilizopo katika ukanda wa Kusini, Magharibi na Kaskazini
Magharibi mwa Tanzania hatua itakayosaidia kuongeza idadi ya watalii pamoja na
pato la Taifa.
Kamishna wa
Uhifadhi TANAPA, Dkt. Allan Kijazi aliyasema hayo jana wakati akizungumza
kwenye ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa TANAPA, Wahariri na Wanahabari
Waandamizi unaofanyika jijini Mwanza.
Itakumbukwa
ukanda wa Magharibi mwa Tanzania unahusisha vivutio vilivyo katika mikoa ya
Rukwa, Katavi, Kigoma na Tabora huku ukanda wa Kaskazini Magharibi ukihusisha mikoa
ya Mwanza, Mara, Geita na Kagera. Aidha ukanda wa Kusini unahusisha mikoa ya Mtwara,
Lindi na Mbeya.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: