Wadau wa Sekta Binafsi Kanda ya Ziwa watoa maoni yao kuhusu "Blue Print"
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Taasisi ya
Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imewakutanisha wafanyabiashara kutoka mikoa
mitano ya Kanda ya Ziwa ili kujadili na kutoa maoni yao kuhusu namna ya kuboresha
mwongozo wa uwekezaji maarufu kama “Blue Print” unaolenga kuondoa vikwazo vya
biashara na uwekezaji nchini.
Mkutano huo
wa majadiliano baina ya wadau wa sekta binafsi umefanyika leo Julai 10, 2019 jijini Mwanza ukiwa
ni mkutano wa pili baada ya ule uliofanyika jijini Dodoma Mei 20, 2019 ambapo
jumla ya mikutano minane inatarajiwa kufanyika katika Kanda nane nchini ili
kutoa fursa kwa wafanyabiashara kutoa maoni yatakayosaidia kuondoa vikwazo vya
biashara na uwekezaji.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye akizungumza kwenye mkutano huo.
Mfanyabiashara jijini Mwanza, Kheri Amran akitoa maoni yake kwenye mkutano huo.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: