LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wafanyabiashara waliokimbia Tanzania watakiwa kurejea

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe amewakaribisha wafanyabiashara ndani na nje ya nchi kutumia fursa ya usafirishaji mizigo kupitia Ushoroba wa Kati (Central Corridor) unaohusisha njia ya reli na bandari.

Mhandisi Kamwelwe ameyasema hayo leo Julai 30, 2019 wakati akizungumza kwenye hafla ya usafirishaji wa mabehewa ya mizigo kwa kutumia meli ya MV. Umoja kupitia Ziwa Victoria kutokea bandari ya Mwanza Kusini (Tanzania) hadi bandari ya Portbell (Uganda), uliofanyika katika bandari ya Mwanza Kusini.

Kwa mara ya kwanza safari ya usafirishaji mizigo ilizinduliwa Juni 24, 2018 ikiwa ni miaka 10 tangu isitishwe katika bandari ya Mwanza Kusini (Tanzania) hadi bandari ya Portbell (Uganda) ambapo hatua hiyo tayari imeanza kuleta tija ya gharama nafuu kwa wanaosafirishaji.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.