LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mkurugenzi alivyopiga simu juu akitatua mgogoro wa ardhi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba amekutana na wananchi pamoja na Mwekezaji kampuni ya Nyakato Interprises ili kusikiliza na kutatua mgogoro wa ardhi walionao ukihusisha kiwanja namba 47 block KKK Nyakato.

Katika mgogoro huo, wananchi wanataka Mwekezaji huyo awalipe fidia kwa thamani ya sasa pamoja na kuwatafutia viwanja maeneo mengine ili wapishe maeneo waliyopo ambapo baada Kibamba kusikiliza pande zote Jumanne Agosti 06, 2019 walikubaliana kukutana tena Ijumaa Agosti 09, 2019 Kamishna wa Ardhi Kanda ya Ziwa akiwepo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba akionesha hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu kuhusu mgogoro wa ardhi baina ya wakazi 25 wa Mhandu na Mwekezaji kampuni ya Nyakato Interprises.
Baadhi ya wakazi wa Mhandu ambao wana mgogoro wa ardhi na Mwenyekezaji kampuni ya Nyakato Interprises.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.