Wadau mkoani Geita wakutana kujadili mikakati ya kupambana na Malaria
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Chama cha
Watoa Huduma Binafsi za Afya Tanzania (APHFTA) kimewakutanisha wadau wanaotekeleza
afua mbalimbali za kupambana na ugonjwa wa Malaria mkoani Geita ili kwa pamoja
kujadili mikakati ya kupambana na ugonjwa huo.
Juhudi za
Serikali na wadau mbalimbali ikiwemo taasisi ya APHFTA inayotekeleza mradi wa
kupambana na Malaria mkoani Geita zimesaidia kiwango cha maambukizi mkoani humo
kupungua kutoka asilimia 38.1 mwaka 2015/16 hadi asilimia 17.3 mwaka 2017/18
ambapo lengo ni kufikia chini ya asilimia tano ifikapo mwaka 2020.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkurugenzi wa Miradi kutoka taasisi ya APHFTA, Elizaberth Bonareri akitoa mrejesho wa utekelezaji wa mradi wa kupambana na Malaria mkoani Geita katika kipindi cha mwaka 2017/19.
Wadau wanaotekeleza afua mbalimbali za kupambana na Malaria mkoani Geita wakifuatilia mada kwenye kikao hicho.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: