LIVE STREAM ADS

Header Ads

Taasisi ya APHFTA yatoa bilioni 1.4 kwa watoa huduma za afya mkoani Geita

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
 Chama cha Watoa Huduma za Afya Binafsi Tanzania (APHFTA) kupitia taasisi yake ya kifedha “Afya Microfinance” kimetoa shilingi bilioni 1.4 kama mikopo kwa watoa huduma za afya mkoani Geita ili kuboresha zaidi huduma zao.

Mkurugenzi wa Miradi kutoka APHFTA, Elizabert Bonareri aliyasema hayo Agosti 26, 2019 wakati akielezea mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa kupambana na Malaria mkoani Geita katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

Ni baada ya wawakilishi kutoka taasisi za Comic Relief na GSK zinazofadhili mradi huo kutembelea huduma mbalimbali zilizoboreshwa kupitia taasisi ya APHFTA ikiwemo Maabara, Vituo vya Afya, Zahanati pamoja na Maduka ya Dawa Muhimu katika Mkoa wa Geita.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Wawakilishi kutoka Comic Relief & GSK wakiwa kwenye moja ya duka la dawa muhimu mkoani Geita lililonufaika na mkopo kutoka APHFTA.
Taasisi ya APHFTA inahimiza watoa huduma za afya kuwa wanachama ili kunufaika na mikopo mbalimbali ili kuboresha huduma zao.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.