LIVE STREAM ADS

Header Ads

Shirika la KIVULINI lawezesha utekelezaji wa MTAKUWWA mkoani Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Shirika la kutetea haki za wasichana na wanawake KIVULINI limekabidhi kompyuta mpakato (Laptops) 10 katika idara mbalimbali za Serikali mkoani Mwanza ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji mkakati wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa watoto na wanawake (MTAKUWWA).

Zoezi la kukabidhi kompyta hizo zenye thamani ya shilingi milioni 12 limefanyika Agosti 27, 2019 kwenye mafunzo kwa wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Watoto na Wanawake Mkoa Mwanza.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la KIVULINI, Yassin Ally amesema zitasaidia uwekaji kumbukumbu na utoaji taarifa na tathmini ya utekelezaji wa MTAKUWWA huku pia shirika hilo likiwa limesaidia uimarishaji mfumo wa utunzaji kumbukumbu (Data Base) ngazi ya Mkoa Mwanza pamoja na Wilaya Misngwi.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Dkt. Christopher Kadio akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Watoto na Wanawake Mkoa Mwanza.
Viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya Misungwi, Juma Sweda (katikati) wakiwa meza kuu kufuatilia mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la KIVULINI, Yassin Ally akisisitiza jambo kwenye mafunzo hayo.
Washiriki wakifuatilia mada kwenye mafunzo hayo.
Tazama BMG Online TV hapa chimi

No comments:

Powered by Blogger.