LIVE STREAM ADS

Header Ads

Binti aliyepoteza miguu, vidole vya mikono na kizazi ashangaza wengi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Binti Asia Patrick mkazi wa Bwiru Wilaya Ilemela mkoani Mwanza aliyepoteza miguu, vidole tisa vya mikono pamoja na kizazi kutokana na matatizo ya uzazi, ameonesha matumaini makubwa ya kutimiza na ndoto zake maishani baada ya kupata viungo bandia.

Ni baada ya binti huyo kuwa mmoja kati ya wa wanufaika wa Kituo cha kutengeneza viungo bandia vya binadamu cha Mwanza Prosthetics & Orthotics Workshop kilichopo Pasiansi wilayani wilayani Ilemela.

Septemba 18, 2019 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella alitembelea Kituo hicho na kukutana na binti Asia ambapo alifurahishwa na ucheshi wake licha ya hali aliyonayo na kuahidi kumuongezea mtaji kwa ajili ya kuanzisha biashara ya saloni pindi atakapohitimu mafunzo yake ya urembo.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.