LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mkandarasi afanikiwa kudhibiti mkondo wa maji “ghorofa lajengwa kwa kasi”

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkandarasi kampuni ya Mzinga amefanikiwa kudhibiti mkondo wa maji ya Ziwa Victoria yaliyokuwa yanakwamisha kasi ya ujenzi wa jengo la ghoroma mbili kwa ajili ya wodi ya wanaume katika Hospitali ya Wilaya Nyamagana “Butimba” mkoani Mwanza.

Serikali ilitenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa wodi hiyo ulioanza mwaka 2017 kwa kusuasua kutokana na mkondo huo wa maji hatua iliyosababisha mabadiliko ya mchoro kufanyika na hivyo Halmashauri ya Jiji la Mwanza kusimamia gharama zilizoongezeka.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Christopher Kadio pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba ametembelea ujenzi wa wodi hiyo inayotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Disemba, 2019.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini

Madiwani wa Jiji la Mwanza wakagua miradi mbalimbali ya maendeleo
#PamojaDaimaBMG

No comments:

Powered by Blogger.