LIVE STREAM ADS

Header Ads

Filimbi yapulizwa Tamasha la Urithi (Urithi Festival 2019) jijini Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella ametembelea maonesho ya Tamasha la Urithi (Urithi Festival 2019) katika viunga vya Rock City Mall jijini Mwanza, lililoanza Oktoba 31, 2019 likitarajiwa kuhitimishwa Novemba 02, 2019 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Tamasha la Urithi 2019 kitaifa mkoani Mwanza linaandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza.
Picha na George Binagi-GB Pazzo, BMG

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto) akicheza mchezo wa bao alipotembelea mabanda kwenye Tamasha la Urithi 2019 jijini Mwanza.

Tamasha la Urithi linalenga kuutangaza utamaduni wa Mtanzania pamoja na Vivutio mbalimbali vya Utalii.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akiwasili kwenye tamasha hilo akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa Mwanza akisalimiana na maafisa mbalimbali alipotembelea banda la Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ambalo ni mdhamini mkuu wa tamasha la Urithi 2019.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akisaini kitabu cha wageni.

Viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella wakifuatilia ngoma mbalimbali za asili kwenye tamasha hilo.

Viongozi wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Urithi 2019 jijini Mwanza wakifuatilia ngoma mbalimbali za asili.

Katibu Tawala Msaidizi Mkoa Mwanza, Emil Kasagala akitoa salamu kwenye tamasha hilo.

Mwenyekiti wa Watemi wa Usukuma akitoa salamu zake kwenye tamasha hilo.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akisalimiana na mwimbaji wa nyimbo za asili, Saida Karoli.

Mwimbaji Saida Karoli akisalimiana na viongozi mbalimbali meza kuu.

Kikundi cha nyimbo za asili kutoka mkoani Kagera kikitumbuiza kwenye tamasha hilo.

Buruzani ya ngoma za asili ikiendelea.

Burudani ya kuvutia ikiendelea.

Ni ubunifu tu kunogesha tamasha la Urithi.

Kikundi cha ngoma asilia kutoka kwa Saida Karoli kikitumbuiza.

Mwimbaji Saida Karoli na kikundi chake akitumbuiza kwenye tamasha hilo.

Saida Karoli akitumbuiza kwenye tamasha hilo.

Saida Karoli.

Kijana akituzwa baada ya kuonesha ubunifu wa kumeza vitu mbalimbali ikiwemo chupa.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (katikati) pamoja na viongozi mbalimbali wakifurahia burudani kwenye tamasha hilo.

Kijana huyu alikuwa kivutio kikubwa kwa uwezo wake wa kumeza vitu mbalimbali ikiwemo misumari, chupa na betri.

Kijana akikaguliwa kama kweli kameza betri....NI KWELI KAMEZA hahahahaaaaa ni ubunifu tu wa utamaduni wa Mtanzania.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye tamasha hilo ikiwa ni siku ya kwanza.

Kilele cha Tamasha la Urithi ni Novemba 02, 2019 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Karibu Tamasha la Urithi wa Mtanzania katika viunga vya Rock City Mall jijini Mwanza, hakuna kiingilioni.

Mmoja wa wadau wakubwa wa Utalii mkoani Mwanza, Matia Levi akifuatilia tamasha hilo ambalo pia limesheheni burudani na bidhaa mbalimbali za asili.

Baada ya Tamasha la Urithi 2019 kufikia tamati Novemba 02, 2019 itafuatia safari ya kuelekea kwenye hifadhi ya Burigi Chato Novemba 03, 2019.

No comments:

Powered by Blogger.