RC Mwanza atangaza Kamati za Maandalizi ya Sherehe za Uhuru 2019
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa
Mwanza, John Mongella ametangaza Kamati tisa zilizopendekezwa kushiriki kwenye Maandalizi
ya Sherehe za Maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika kwa mwaka 2019
zinazotarajiwa kufanyika kitaifa jijini Mwanza.
Mongella
ametaja Kamati hizo pamoja na viongozi na wajumbe waliopendekezwa mbele ya
kikao cha kwanza cha maandalizi ya sherehe hizo kilichojumuisha pia wajumbe wa
Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa Mwanza (KUU) kabla ya mapendekezo hayo
kufikishwa katika Kamati ya kitaifa.
Mongella amezitaka Kamati zilizopendekezwa kuwa ni Burudani Habari na Uhamasishaji, Halaiki, Afya Usafi na Mazingira, Chakula, Fedha na Uwezeshaji, Usafiri Mapokezi na Itifaki, Miundombinu, Sare Mabango na Mapambo pamoja na Usalama.
Kikao hicho cha
kwanza cha Maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika zinazotarajiwa
kuanza Disemba 02, 2019 hadi Disemba 09, 2019 kimefanyika katika ukumbi wa
mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, Nove,ba 12, 2019.
Itakumbukwa
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli alitangaza rasmi Sherehe za Uhuru 2019 kufanyika kitaifa
jijini Mwanza wakati akizungumza kwenye Baraza la Maulid 2019 lililofanyika
kitaifa pia jijini Mwanza, Novemba 10, 2019.
Kikao cha kwanza cha maandalizi ya Sherehe za Uhuru 2019 kilichofanyika jijini Mwanza.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini
No comments: