LIVE STREAM ADS

Header Ads

TANZANIA "bilioni 179 kutekeleza mradi wa Ujazilizi katika mikoa tisa"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imetenga shilingi bilioni 179 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa Ujazilizi katika mikoa tisa nchini ukiwemo Mwanza kuanzia mwezi Januari 2020.

Mgalu aliyasema hayo Disemba 22, 2019 wakati akijibu malalamiko ya wakazi wa Kata ya Kayenze iliyopo Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza waliolalamika kutofikiwa na nishati ya umeme kupitia mradi wa REA.

Aidha Mgalu ambaye pamoja na shughuli nyingine aliwasha umeme katika maeneo mbalimbali ikiwemo Shule ya Msingi Lutongo, alibainisha kwamba mradi huo wa Ujazilizi utafikisha umeme katika maeneo yote ambayo hayakufikiwa na nishati hiyo kupitia mradi wa REA.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.