Wazee wa mila wakubali kushiriki mapambano dhidi ya Ukatili wa Kijinsia
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Wazee wa
mila kutoka mikoa tisa nchini yenye kiwango kikubwa cha ukatili wa kijinsia
wamekubaliana kutumia ushawishi walio nao ili kwenye mapambano dhidi ya vitendo
hivyo ikiwemo ukeketaji, kutakasa wanawake, mimba na ndoa za utotoni.
Wazee hao
wamefikia maazimio hayo Disemba 05, 2019 jijini Mwanza kwenye mkutano
ulioshirikisha viongozi wa mila zaidi ya 200 kutoka makabila mbalimbali ya
mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Geita, Kagera, Simiyu, Tabora, Katavi na
Manyara ulioandaliwa na shirika la UN Women.
Hata hivyo mmoja
wa wazee hao, Chifu Mfungo Charles kutoka mkoani Geita amesema changamoto
waliyonayo ni kukosa nguvu kisheria na hivyo kuomba Serikali kuwarejeshea mamlaka
waliyokuwa nayo hatua itawaongezea nguvu ya kupambana na yeyote atayekumbatia mila
zinazochochea ukatili wa kijinsia.
Kwa upande
Mkuu wa kitengo cha kupambana na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto wa
kike kutoka shirika la UN Women, Lucy Tesha amesema wazee wa mila ni wadau
muhimu katika kutokomeza mila na desturi zinazorudisha nyuma maendeleo ya
wanawake hivyo kuwashirikisha kwenye mapambano hayo kutasaidia kuleta
mabadiliko katika jamii zao ikiwemo kuwashirikisha wanawake katika shughuli za
kiuchumi.
Itakumbukwa
mikoa yenye kiwango kikubwa cha ukatili nchini ni Mara asilimia 78, Shinyanga
asilimia 78, Tabora asilimia 71, Kagera asilimia 67, Geita asilimia 63, Simiyu
asilimia 62, Kigoma asilimia 61, Mwanza asilimia 60, Njombe asilimia 53, Dodoma
asilimia 50 na Katavi asilimia 50.
Mkuu wa kitengo cha kupambana na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto wa kike kutoka shirika la UN Women, Lucy Tesha akiwahimiza wazee wa mila kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Geita, Kagera, Simiyu, Tabora, Katavi na Manyara kutumia ushawishi wao katika jamii kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wazee wa mila kutoka mikoa tisa nchini yenye kiwango kikubwa cha ukatili wa kijinsia wakifuatilia mkutano huo.
Mkuu wa kitengo cha kupambana na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na wasichana kutoka shirika la UN Women, Lucy Tesha akifafanua jambo kwa wazee wa mila waliohudhuria mkutano huo.
Wazee wa Mila kutoka mikoa tisa nchini yenye kiwango kikubwa cha vitendo vya ukatili wa kijinsia wakiwa kwenye mkutano wa kujengeana uwezo na kuweka mikakati ya kutokomeza vitendo hivyo.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini
No comments: