RC Mongella azindua zoezi la upuliziaji dawa ya ukoko wilayani Ukerewe
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Mkoa
Mwanza, John Mongella amezindua rasmi zoezi la upuliziaji dawa ya ukoko katika
makazi na mazalia ya mbu wilayani Ukerewe ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa
afua mbalimbali za kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa Malaria.
Akizungumza
Machi 09, 2020 na wakazi wa Kata ya Ngoma baada ya kuzindua zoezi hilo,
Mongella aliwahimiza wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwani dawa hiyo
haina madhara yoyote kwa binadamu.
Serikali
inashirikiana na taasisi ya “ABT Associates” kutekeleza mradi wa unyunyiziaji
dawa ya kuua mazalia ya mbu (PMI VectorLink) kupitia ufadhili wa wadau
mbalimbali ikiwemo US Aid, CDC pamoja na mfuko wa kupambana na Malaria wa Rais
wa Marekani.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akinyunyizia dawa ya ukoko kwa ajili ya kuua mazalia ya mbu katika nyumba ya mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Hamkoko wilayani Ukerewe.
Tazama BMG TV hapa chini
No comments: