LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wakazi wa Misungwi kupata huduma bora za Uzazi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

 Zaidi ya wakazi elfu sabini (wakazi 71,960) hususani akina mama wajawazito na watoto katika Tarafa ya Mbarika Wilaya Misungwi mkoani Mwanza, wanatarajia kunufaika na huduma bora za uzazi baada ya kukamilika kwa ujenzi wa wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Mbarika.

Hayo yalielezwa kwenye hafla ya kukabidhi jengo la wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Mbarika lililojengwa kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la nchini Canada (Global Affair) kupitia mradi wa Mama na Mtoto uliokuwa unatekelezwa wilayani Misungwi kuanzia mwaka 2016.
 Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mbarika, Dkt. Barnabas Makanza alisema jengo hilo limegharimu shilingi Milioni 156 hadi kukamilika ambapo Shirika la Global Affair lilitoa shilingi Milioni 146, Halmashauri wa shilingi Milioni tano huku wanajamii wakichangia mawe, mchanga pamoja na nguvu kazi ya kuchimba msingi  na maji na hivyo kufanya mchango wao kufikia thamani ya shilingi Milioni tano.

Dk. Makanza alibainisha kwamba Jengo hilo lina uwezo wa kuwekwa vitanda 31 vya kuhudumia wazazi  wanne  kwa wakati mmoja pamoja na uwezo wa vitanda vinne vya kujifungulia (derivery beds).
 Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Misungwi Juma Sweda, Afisa Tawala Wilaya ya Misungwi Zubeda Kimario aliwataka wananchi wa Tarafa ya Mbarika kuitunza vyema wodi hiyo ili kusaidia mapambano dhidi ya vifo vya akina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Naye Mganga Mkuu Wilaya ya Misungwi, Dkt. Zabron Masatu alisema Tarafa ya Mbarika Wilayani Misungwi ni moja kati ya maeneo yaliyokuwa yameshamiri vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano kutokana na adha ya kukosekana kwa  huduma za uzazi.
 Kwa upande wake Meneja Mradi wa mama na mtoto, Tanya Salewski alisema mradi wa Mama na Mtoto umesaidia kuimarisha huduma za uzazi kwa akina mama na watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi tangu mwaka 2016 na kufanikiwa kujenga jengo la upasuaji, kutoa gari la wagonjwa (Ambulance) ambalo pamoja na ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje katika Zahanati ya Nyamayinza na ukarabati wa chumba cha upasuaji mdogo katika Zahanati ya Mwawile.
 Kupitia Mradi wa Mama na Mtoto, Halmashauri ya Wilaya Misungwi pia imepokea gari aina ya Toyati Nissan yenye thamani ya shilingi Milioni  140 kwa ajili ya kusaidia uboreshaji wa shughuli za afya wilayani humo.
Tazama BMG TV hapa chini
#BMGHabari

No comments:

Powered by Blogger.