LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wasiojiweza wasaidiwa gharama za matibabu katika Hospitali ya Bugando

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

 Baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika Shule ya Sekondari Makoko Seminari (Makoko Seminary) iliyopo Musoma mkoani Mara, wametoa msaada wa fedha ili kusaidia gharama za matibabu kwa wagonjwa wenye uhitaji katika Hospitali ya Kanda Bugando jijini Mwanza.

Waseminari hayo walikabidhi msaada huo kwa niaba ya wenzao Jumatatu Aprili 13, 2020 huku ikielezwa kuwa gharama za wagonjwa wasiojimudu kiuchumi ambao wanaoomba msamaha wa matibabu katika hospitali ya Bugando zinafikia milioni 200 kila baada ya miezi mitatu hivyo ni vyema wadau mbalimbali wakaendelea kusaidia upatikanaji wa gharama hizo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Badhi ya wanafunzi waliowahi kusoma Shule ya Sekondari Makoko Seminari (Makoko Seminary) iliyopo Musoma mkoani Mara wakifanya maombi baada ya kuwasili katika Hospitali ya Kanda Bugando kuwasilisha msaada wa fedha kwa ajili ya kugharamia matibabu kwa wagonjwa wenye uhitaji.
 Badhi ya wanafunzi waliowahi kusoma Shule ya Sekondari Makoko Seminari (Makoko Seminary) iliyopo Musoma mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa Hospitali ya Kanda Bugando baada ya kukabidhi msaada wa fedha katika Hospitali hiyo kwa ajili ya kusaidia gharama za matibabu kwa wagonjwa wasiojimudu kiuchumi.
Badhi ya wanafunzi waliowahi kusoma Shule ya Sekondari Makoko Seminari (Makoko Seminary) iliyopo Musoma mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa Hospitali ya Kanda Bugando.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.