LIVE STREAM ADS

Header Ads

Benki ya NCBA yaja na mapinduzi makubwa Tanzania

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Benki mpya ya NCBA imewaahidi wateja wake upatikanaji wa huduma bora za kifedha ikiwemo mikopo yenye riba na masharti nafuu ili kuhakikisha wanatimiza safari yao ya mafanikio.

Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya NCBA, Margareth Karume (juu) aliyasema hayo jijini Mwanza Oktoba 02, 2020 kwenye hafla ya jioni (mchapalo) ya uzinduzi wa matawi mawili ya benki hiyo iliyofanyika Malaika Hoteli. 

Benki ya NCBA imetokana na muunganiko wa benki mbili ambazo ni NIC na CBA uliofanyika Julai 08, 2020 ambapo tayari imezindua matawi yake katika mikoa ya Dar, Arusha, Mwanza na Zanzibari huku pia ikiwa na matawi katika nchi mbalimbali barani Afrika.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMGMkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchapalo huo alisema matarajio ni kuona benki ya NCBA ikitoa msukumo wa maendeleo kwa wananchi hapa nchini.Mkurugenzi wa biashara ndogo, za kati na kubwa kutoka benki ya NCBA, Gift Shoko akizungumza kwenye mchapalo uliowahusisha wateja wa benki hiyo Ijumaa Oktoba 02, 2020 jijini Mwanza.Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.