LIVE STREAM ADS

Header Ads

MKUU WA WILAYA MISUNGWI AZINDUA MSIMU MPYA WA PAMBA

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Wilaya Misungwi mkoani Mwanza, Juma Sweda amezindua rasmi msimu mpya wa kupanda zao la pamba kwa mwaka 2020/21 na kutumia fursa hiyo kuwaelekeza Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kuwakamata watakaokutwa vijiweni muda wa kazi.

Sweda akiwa ameambatana na viongozi na watendaji mbalimbali wilayani Misungwi, alizundua msimu huo Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Maganzo Kata ya Mondo na kusisitiza kwamba wananchi wote wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo. 

Alisema kila mwenye shamba lazima akalime kwani ni aibu kukuta vijana wanacheza bao, karata ama kunywa pombe muda wa shamba huku wengine hususana akina mama wakiwa mashambani. 

“Wakamatwe wapelekwe wakalime, ikifanyika hivyo kila mtu atafanya kazi kwa bidii kwa sababu hakuna wa kuja kukusaidia” alisisitiza Sweda. 
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Wilaya Misungwi, Juma Sweda akipanda pamba akiwa na watendaji pamoja na wakulima katika Kata ya Mondo kwenye uzinduzi wa msimu mpya wa zao la pamba ulioanza Novemba 15 hadi Disemba 15, 2020.
Mkuu wa Wilaya Misungwi, Juma Sweda akilima kwa jembe la kukokotwa na ng'ombe  ikiwa ni maandalizi ya kupamba pamba.
Katibu Tawala Wilaya Misungwi, Petro Sabatto ni miongoni mwa viongozi walioshiriki kuhamasisha msimu wa ulimaji pamba 2020/21.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.