LIVE STREAM ADS

Header Ads

Maajabu!! Milima ya kustaajabisha mkoani Mara (sehemu ya 01)

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Ni mwonekano wa milima ambayo inapatikana katika Wilaya ya Rorya mkoani Mara, mita chache kutoka mto Mara ukiwa unatoka ama unaelekea Wilayani Tarime, ukitokea maeneo mbalimbali katika barabara ya Musoma-Tarime. 

Maajabu ya milima ambayo iko pande zote mbili za barabara si kwamba yanatisha, la hasha. Ni maajabu ambayo ni ya kufurahisha kiukweli hususani ukiwa safarini ambapo ukiitazama utaona namna inavyorudi nyumba na kufanya abiria kuhisi uumbaji wa Mungu uliotukuka katika hii dunia. 

Ujenzi wa barabara iliyopinda mithiri ya nyoka katikakati ya milima hii huifanya kuwa kivutio kingine japo kwa abiria waoga wakifika katika milima hii sara huwa inaongezeka maana si mchezo hususani likija suala la mpando huwa ni mpando kweli, na likija suala la mteremko huwa ni mteremko kweli kwani ikiwa wewe ni muoga basi huweza hata chungulia nje japo ukweli ni kwamba ukichungulia nje utaona uzuri wa kipekee katika milima hiyo. 

Kikubwa tunaomba shughuli za kibidanamu zisiiathiri milima hii maana ni tegemeo kwa wanamara na sote twajua umuhimu wa milima kama hii ambayo ina uwepo mkubwa wa misitu ya asili.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.