Tuzo za 'Mwanamke Kinara' Kanda ya Ziwa kutolewa jijini Mwanza
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani 2021, taasisi ya 'Women Round Table' imeandaa tuzo za Mwanamke Kinara kwa ajili ya kutambua jitihada za wanawake kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa Jumapili Machi 07, 2021 jijini Mwanza kwenye kongamano la wanawake la 'Women Round Table' litakalofanyika Gold Crest Hotel kuanzia majira ya saa nne asubuhi ikiwa ni siku moja kabla ya kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani itakayoadhimishwa Machi 08, 2021.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Tazama BMG TV hapa chini
SOMA>>> Habari zaidi hapa
No comments: