Makamu wa Rais alivyowasili Mwanza kwa ajili ya jambo hili zito
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango (kushoto) akisalimiana na viongozi mbalimbali mkoani Mwanza baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza.
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango (kushoto) akiwasili jijini Mwanza, Katikati ni Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Simiyu)
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango akitoa salamu kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa ibada ya kumsimika Askofu wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza.
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango akizungumza kwenye ibada hiyo.
Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dkt. Maimbo Mndolwa akizungumza wakati wa ibada hiyo.
Ibada ya kumsimika Askofu Mteule wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza, Zephania Ntunza (wa kwanza mbele).
Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dkt. Maimbo Mndolwa akiongoza zoezi la kumsimika Askofu wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza, Zephania Ntunza.
Ibada ya kumsimika Askofu wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza, Zephania Ntunza.
Askofu wa Kanisa Katoliki Dayosisi ya Mwanza, Renatus Nkwande akitoa salamu wakati wa ibada hiyo.
Sheikh wa Mkoa Mwanza, Hassan Kabeke akitoa salamu wakati wa ibada hiyo na kumtakia heri Askofu wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza, Zephania Ntunza.
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango na viongozi mbalimbali wa dini wakiwa kwenye ibada hiyo.
Waamini wa Kanisa Anglikana wakifuatilia ibada hiyo.
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Kanisa Anglikana.
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Kanisa Anglikana Tanzania.
Tazama BMG TV hapa chini
No comments: