LIVE STREAM ADS

Header Ads

KAHAMA: Wajumbe wa Bodi SHUWASA wakagua mradi wa maji Ngogwa-Kitwana

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA Mhandisi Yusuph Katopola (kushoto) akielezea kuhusu Mradi wa ujenzi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama unaosimamiwa na kutekelezwa na SHUWASA wakati wajumbe wa Bodi ya SHUWASA walipotembelea na kukagua mradi huo Jumanne Agosti 17, 2021.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Bodi ya Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) imetembelea na kukagua utekelezaji wa ujenzi wa Mradi wa Maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama unaosimamiwa na kutekelezwa na SHUWASA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Kahama (KUWASA) na Wakala wa Usambazaji Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Shinyanga na Wilaya ya Kahama.

Wajumbe hao wa Bodi ya SHUWASA wametembelea mradi huo leo Jumanne Agosti 17,2021 na kujionea maendeleo ya ujenzi wa mradi huo wenye gharama ya shilingi Bilioni 2.4 unaotarajiwa kukamilishwa ifikapo Mwezi Oktoba ,2021.

Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA, Bi. Mwamvua Jilumbi amesema maendeleo ya ujenzi huo yanaridhisha huku akibainisha kuwa mradi huo uliopaswa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2020 ulikwama kutokana changamoto ya upatikanaji wa mabomba.

“Tulikumbwa na changamoto ya upatikanaji wa mabomba ambapo Mzabuni tuliyeingia naye mkataba badala ya kuleta mabomba tuliyokubaliana yeye alileta mengine tu yasiyohusika. Tulivunja mkataba naye tukatafuta mzabuni mwingine ambaye sasa analeta mabomba ya chuma na tunatarajia ifikapo Mwezi Oktoba 2021 wananchi wataanza kupata huduma ya maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria”,amesema Jilumbi.

Amesema lengo la serikali ni kuhakikisha inawatua ndoo vichwani akina mama hivyo pindi mradi huo utakapokamilika utasaidia wananchi kuondokana na kero ya muda mrefu ya ukosefu wa maji safi na salama na kujikuta wakilazimika kutembea umbali mrefu kutafuta maji kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA Mhandisi Yusuph Katopola amesema mradi huo unaojengwa kwa kutumia Wataalamu wa ndani ‘Force Account’ unajengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 2.4 na unatarajiwa kunufaisha wananchi zaidi ya 27,000 pindi utakapokamilika mwezi Oktoba 2021.

“Mradi huu unahusisha ujenzi matanki mawili katika maeneo ya Ngogwa na Kitwana. Ujenzi tanki la Ngogwa lenye ujazo wa lita za ujazo 680,000 umekamilika na lile la Kitwana lenye ujazo wa lita 135,000 ujenzi wake uko mbioni kukamilika na tupo kwenye hatua za ukamilishaji ujenzi wa maghati 14 ya kuchotea maji”,amesema Mhandisi Katopola.

Ameeleza kuwa licha ya SHUWASA kuhudumia kata zote 17 za Manispaa ya Shinyanga kwa kuzipatia huduma ya maji safi na salama, Serikali iliiteua SHUWASA kusimamia ujenzi wa mradi wa maji wa Ngogwa - Kitwana kwa vile ndiyo Mamlaka ya Maji ya Mkoa wa Shinyanga ambapo baada ya kukamilika kwa mradi, Mamlaka ya Maji ya Mji wa Kahama (KUWASA) ndiyo itakayoendelea kusimamia mradi huo.
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA Mhandisi Yusuph Katopola (kushoto) akielezea kuhusu Mradi wa ujenzi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama unaosimamiwa na kutekelezwa na SHUWASA wakati wajumbe wa Bodi ya SHUWASA walipotembelea na kukagua mradi huo leo Jumanne Agosti 17,2021.
Muonekano wa ghati la maji katika Senta ya Kitwana kwenye Mradi wa ujenzi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama unaosimamiwa na kutekelezwa na SHUWASA.
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA Mhandisi Yusuph Katopola (wa pili kulia) akiwaonesha ghati la maji katika Senta ya Kitwana kwenye Mradi wa ujenzi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama unaosimamiwa na kutekelezwa na SHUWASA wakati wajumbe wa Bodi ya SHUWASA wakitembelea na kukagua mradi huo.
Msimamizi wa Ujenzi wa Mradi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama, Mhandisi Hassan Kassim Fussi akielezea kuhusu ujenzi wa maghati 14 ya kuchotea maji wakati wajumbe wa Bodi ya SHUWASA walipotembelea na kukagua mradi huo.
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA Mhandisi Yusuph Katopola (kulia) akiwaelezea wajumbe wa Bodi ya SHUWASA kuhusu ujenzi maghati la kuchotea maji unaoendelea katika Mradi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA Bi. Mwamvua Jilumbi.
Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA Bi. Mwamvua Jilumbi (katikati) na wajumbe wa bodi ya SHUWASA wakiangalia shughuli ya ujenzi wa maghati ya kuchotea maji katika Mradi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama.
Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA Bi. Mwamvua Jilumbi (katikati) na wajumbe wa bodi ya SHUWASA wakiangalia shughuli ya ujenzi wa maghati ya kuchotea maji katika Mradi wa maji wa Ngogwa – Kitwana wilayani Kahama.
Wajumbe wa bodi ya SHUWASA wakiangalia shughuli ya ujenzi wa tenki la juu kwenye mwinuko ‘riser’ wa mita 12 lenye ukubwa wa lita 135,000 katika kijiji cha Kitwana
Muonekano hatua ya ujenzi wa tenki la juu kwenye mwinuko ‘riser’ wa mita 12 lenye ukubwa wa lita 135,000 katika kijiji cha Kitwana.
Wajumbe wa bodi ya SHUWASA wakiangalia shughuli ya ujenzi wa tenki la juu kwenye mwinuko ‘riser’ wa mita 12 lenye ukubwa wa lita 135,000 katika kijiji cha Kitwana
Wajumbe wa bodi ya SHUWASA wakiangalia shughuli ya ujenzi wa tenki la juu kwenye mwinuko ‘riser’ wa mita 12 lenye ukubwa wa lita 135,000 katika kijiji cha Kitwana
Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA Bi. Mwamvua Jilumbi (katikati) akizungumza katika Tenki la Maji la Kitwana lenye ujazo wa lita 135,000
Wajumbe wa bodi ya SHUWASA wakiwa katika kata ya Busoka ambapo bomba la maji ya Mradi wa Ngogwa - Kitwana litapita eneo la barabara.
Muonekano ujenzi wa ghati la kuchotea maji katika Shule ya Msingi Ngogwa kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Mhandisi wa Mipango na Ujenzi kutoka SHUWASA, Wilfred Julius akielezea kuhusu ujenzi wa tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA Mhandisi Yusuph Katopola akiongoza wajumbe wa Bodi ya SHUWASA na wadau wengine kupanda Mlima Ngogwa wenye urefu wa mita 280 ili kwenda kuona tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA , Bi. Mwamvua Jilumbi (kulia) akipanda Mlima Ngogwa wenye urefu wa mita 280 ili kwenda kuona tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA Bi. Mwamvua Jilumbi akipanda katika tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Muonekano tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Kaimu Mkurugenzi wa SHUWASA, Mhandisi Yusuph Katopola (mwenye suti ya bluu) akishuka katika tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya SHUWASA Bi. Mwamvua Jilumbi (mbele) na wajumbe wa Bodi ya SHUWASA wakiondoka katika tenki la kukusanyia maji la ardhini ‘Ground water tank’ lenye ukubwa wa lita 680,000 katika kijiji cha Ngogwa kata ya Ngogwa.

No comments:

Powered by Blogger.