LIVE STREAM ADS

Header Ads

TAKUKURU yabaini mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Online Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kukupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Singida, Mzalendo Widege akitoa taarifa kwa vyombo vya habari ya namna walivyotekeleza majukumu ya uzuiaji wa vitendo vya rushwa, uchunguzi na elimu kwa umma, kwa kipindi cha Aprili hadi Juni 2022 Kulia ni Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoani hapa, Adam Kiongozi.
Maafisa wa TAKUKURU wakiwa kwenye mkutano huo wa kutoa taarifa kwa vyombo vya habari.
Mkutano huo ukiendelea.
Taswira ya mkutano huo.


Na Dotto Mwaibale, Singida
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani hapa imebaini mianya mbalimbali ya upotevu wa mapato katika baadhi ya halmashauri sanjari na matumizi ya fedha mbichi kwa visingizio vya changamoto za kimtandao.

Aidha, Taasisi hiyo pamoja na mambo mengine, imefanya chambuzi katika sekta ya madini ya ujenzi, uvuvi na mapato yatokanayo na makusanyo ya POS na kubaini kasoro kubwa za mapato hayo kukatiwa stakabadhi mara mbili sambamba na ucheleweshwaji wa kupelekwa benki.

Hayo yamebainishwa Agosti 10, 2022 na Mkuu wa Takukuru mkoani hapa, Mzalendo Widege wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari ya namna walivyotekeleza majukumu ya uzuiaji wa vitendo vya rushwa, uchunguzi na elimu kwa umma, kwa kipindi cha Aprili hadi Juni 2022.

"Kwenye upande wa makusanyo kuna tatizo la baadhi ya watendaji kutumia fedha mbichi kwa visingizio vya matatizo ya mtandao au umbali wa ofisi za halmashauri" alisema.

Widege alisema katika kipindi hicho taasisi imechukua hatua kadhaa katika kukabiliana na changamoto hiyo ikiwemo kuendesha warsha zilizolenga kuziba mianya ya rushwa na upotevu wa mapato hususani kwenye maeneo ya sekta ya madini na mabaraza ya ardhi ya kata na vijiji.

Pia kwa mujibu Takukuru, katika kipindi hicho wamepokea takribani malalamiko 70 ya taarifa za rushwa na zisizo za rushwa kwenye maeneo ya ardhi, serikali za mitaa, mahakama, elimu, polisi, afya na sekta binafsi na uchunguzi unaendelea.

No comments:

Powered by Blogger.