LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wachimbaji madini 159 nchini, wapoteza maisha migodini, 59 wajeruhiwa

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com

Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Tume ya Madini Dk. Anold Gasase akizungumza wakati akifungua mafunzo yanayowahusisha wachimbaji wadogo wa kanda ya kati yanayofanyika mkoani hapa. Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Tume ya Madini yameanza Januari 26, 2023 na yatafikia tamati Januari 27, 2023. 

Na Dotto Mwaibale, Singida

WACHIMBAJI wadogo wa madini 139 nchini wamepoteza maisha katika maeneo ya migodi huku 59 wakijeruhiwa katika kipindi cha mwaka 1918 hadi 1919 na 2019-2020.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Tume ya Madini Dk. Anold Gasase wakati akifungua mafunzo yanayowahusisha wachimbaji wadogo wa kanda ya kati yenye lengo la kuelimisha, kukumbushana masuala ya usalama, baruti, uhifadhi wa mazingira katika maeneo ya uchimbaji mdogo yanayofanyika mkoani hapa.

Alisema mafunzo hayo ambayo yanatolewa na wataalam mbalimbali kutoka Tume ya Madini yana lenga kuhakikisha shughuli za uchimbaji wa madini na uchanjuaji wa madini zinafanyika katika mazingira yenye kuzingatia usalama, afya na taratibu na miongozo mbalimbali iliyotolewa.

“Shughuli za uchimbaji na uhanjuaji wa madini zinamanufaa makubwa kwa wachimbaji na taifa kwa ujumla kupitia fursa za ajira, biashara pamoja na kodi mbalimbali” alisema Gasase.

Alisema pamoja na manufaa hayo shughuli hizo zimekuwa zikikutana na matukio ya ajali, madhara ya kiafya, uhalibifu wa mazingira kwenye baadhi ya machimbo na kusa na kusababisha vifo na majeruhi hali ambayo sio afya katika sekta ya madini.

Alisema uchunguzi uliofanyika unaonesha kwamba ajali hizo zinasababishwa na kuanguka kwa mashmo na kuwafukia wachimbaji na kukosekana kwa hewa ndani ya mashimo ya uchimbaji. 

Aidha Gasase alisema tafiti zinaonesha ajali nyingi, athari za kiafya na uhalibifu wa mazingira migodini zinasababishwa na uzingatiaji mdogo na elimu ya masuala ya usalama, afya na utunzaji wa mazingira miongoni mwa wachimbaji.

Alisema shughuli za uchimbaji zinahusisha utunzaji na usafirishaji wa baruti ambazo zinaambatana  na usalama, kiafya na uhalibifu wa mazingira ambapo sheria ya baruti ya mwaka 1963 na kanuni zake za mwaka 1964 zisipozingatiwa na wasambaji na watumiaji wa baruti.

Dk.Gasase alitumia nafasi hiyo kuwaomba washiriki wa mafunzo hayo kujifunza kwamakini na kuuliza maswali ili waweze kujua mambo mbalimbali yanayohusu sheria za uchimbaji na mengineyo.

Mwenyekiti wa wachimbaji wadogo Mkoa wa Singida Robert Malando alisema changamoto kubwa waliyonayo ni kukatika mara kwa mara kwa umeme ambapo waliomba Tume ya Madini na Serikali iwasaidie.

Baadhi ya wachimbaji wa madini waliohudhuria mafunzo hayo wameipongeza Tume ya madini kwa kuwapelekea mafunzo hayo ambayo yamewaongezea uelewa na ujasiri na kuwa  hawataogopa kwenda kulipa kodi tofauti na hap awali alisema Magdalena Lucas ambaye ni mchimbaji wa madini kutoka mgodi wa Mpipiti.

Mada zilizotolewa kwenye mafunzo hayo ni Sheria ya madini, Taratibu za upatikanaji wa leseni kwa wachimbaji wa madini, Taratibu za usimamizi wa mgodi, Usalama na afya migodini na Usimamizi wa baruti.

Mkurugenzi wa Ukaguzi Migodi na Mazingira, Mhandisi Henry Mditi, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo. Kushoto ni Kaimu Afisa Madini Mkoa wa Singida, Elizabeth Mwiza na kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Tume ya Madini Dk. Anold Gasase
Mwenyekiti wa Wachimbaji wadogo wa madini Mkoa wa Singida, Robert Malando akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Mchimbaji mdogo wa madini ambaye aliwawakilisha wachimbaji madini wanawake, Magdalena Lucas akizungumzia manufaa ya mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi. Kutoka kushoto waliokaa ni Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini Tume ya Madini, Venance Kasiki, Mkurugenzi wa Ukaguzi Migodi na Mazingira, Mhandisi Henry Mdit. Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Tume ya Madini, Dk.Anold Gasase, Kaimu Afisa Madini Mkoa wa Singida, Elizabeth Mwiza na Mwenyekiti wa Wachimbaji wadogo wa Madini Mkoa wa Sindida, Robert Malando
Wachimbaji wadogo wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi
Wanawake wachimbaji madini wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.na viongozi wengine wa sekta ya madini.
 

No comments:

Powered by Blogger.