LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kamati ya Bunge yaridhishwa na ujenzi wa kiwanda cha mabomba mradi wa mafuta EACOP

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Wajumbe wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiwa katika kiwanda kitakachokuwa kikiweka mifumo ya upashaji joto na plastiki itakayozuia upotevu wa joto kwenye mabomba yatakayotumika katika mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).
Wajumbe wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiwa katika kiwanda kitakachokuwa kikiweka mifumo ya upashaji joto na plastiki itakayozuia upotevu wa joto kwenye mabomba yatakayotumika katika mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP). 
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakikagua mitambo mbalimbali inayoendelea kufungwa katika kiwanda kitakachokuwa kikiweka mifumo ya upashaji joto na plastiki itakayozuia upotevu wa joto kwenye mabomba yatakayotumika katika mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP). Wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Nishati, Wakili Stephen Byabato. Kiwanda kipo wilaya ya Nzega mkoani Tabora.

Na Mwandishi wetu – Tabora
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imepongeza kasi ya ujenzi wa kiwanda kitakachokuwa kikiweka mifumo ya upashaji joto na plastiki itakayozuia upotevu wa joto kwenye mabomba yatakayotumika katika mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).

Hayo yameelezwa tarehe 26 Agosti, 2023 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Judith Kapinga katika Kijiji cha Sojo, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora wakati wajumbe wa Kamati hiyo walipofika kiwandani hapo kujionea utekelezaji wake.

Baada ya kukagua kazi mbalimbali zinazoendelea katika kiwanda hicho ambacho ujenzi wake kwa ujumla umefikia asilimia 95, Mhe. Kapinga ameipongeza Serikali kwa utekelezaji huo ambapo pia amesifu teknolojia ya hali ya juu inayotumika katika kiwanda hicho.

“Kamati imeridhishwa na maendeleo ya mradi huu ambao kwa kweli unatekelezwa kwa kasi nzuri, nichukue fursa hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan na Serikali kwa ujumla kwa kuendelea kuhakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa ipasavyo” amesema Kapinga.

Kapinga ametoa wito kwa Serikali kuendelea kutoa elimu kwa wananchi hasa wanaozunguka miradi mbalimbali inayoendelea chini ya EACOP kuhusu fursa zinazotokana na miradi hiyo, huduma za kijamii na kuhakikisha kuwa mahusiano chanya na wananchi wanaozunguka miradi yanaendelea kuwepo ili miradi hiyo ifanyike kwa ufanisi.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati, Stephen Byabato pamoja na kueleza hatua zinazoendelea kufanyika katika mradi wa EACOP ikiwemo ujenzi wa kiwanda hicho na kambi mbalimbali zitakazotumika kwa ajili ya wafanyakazi na kuhifadhi vifaa vitakavyotumika wakati wa utekelezaji mradi, amesema kuwa Serikali pia inaendelea kusimamia kwa umakini suala la utoaji wa huduma za kijamii katika maeneo ambapo mradi unapita.

Byabato amewashukuru Wajumbe wa Kamati kwa kufanya ziara hiyo ili kujionea jinsi Serikali inavyoendelea kutekeleza mradi wa EACOP na kuahidi kuwa maoni mbalimbali yaliyotolewa na Wajumbe hao yatafanyiwa kazi na Serikali ili kuendelea kuboresha utekelezaji wa mradi wa EACOP.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitwapaki Tukai amesema kuwa, utekelezaji wa mradi huo unaenda vizuri na kumekuwepo na ushirikishwaji mzuri wa jamii inayozunguka mradi lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa wanafaidika na uwepo wa kiwanda hicho katika eneo la Sojo.

Viongozi mbalimbali waliohudhuria ziara hiyo ni Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitwapaki Tukai, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Mussa Makame, Mratibu Mradi wa EACOP upande wa Tanzania, Asiad Mrutu na Mratibu Mradi wa EACOP katika Wizara ya Nishati, Kisamarwa Nyang’au.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Judith Kapinga.
Naibu Waziri wa Nishati, Wakili Stephen Byabato.
Mitambo mbalimbali inayoendelea kufungwa katika kiwanda kitakachokuwa kikiweka mifumo ya upashaji joto na plastiki itakayozuia upotevu wa joto kwenye mabomba yatakayotumika katika mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).Kiwanda kipo wilaya ya Nzega mkoani Tabora.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakikagua kazi mbalimbali zinazoendelea katika kiwanda hicho.
Wajumbe wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiwa katika kiwanda hicho.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitapwaki Tukai akizungumza wakati Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Mratibu wa mradi wa bomba la mafuta ghafi, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Asiadi Mrutu.
Kiongozi wa Ushirikishwaji wa Watanzania kwenye Mradi wa EACOP, Loi Rogers akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Kiongozi wa Ushirikishwaji wa Watanzania kwenye Mradi wa EACOP, Loi Rogers akizungumza wakati wa ziaa hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Msalala Mkoani Shinyanga, Idd Kassim ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Sengerema mkoani Mwanza, Hamis Tabasamu ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Mwonekano wa sehemu ya kiwanda.

No comments:

Powered by Blogger.