LIVE STREAM ADS

Header Ads

Shirika la JHPIEGO laendesha mbio za hisani kuchangisha fedha za ujenzi wa wodi ya watoto njiti

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Shirika la JHPIEGO Tanzania kwa kushirikiana na taasisi ya Doris Molles limeendesha mbio za hisani za 'Miles For Mothers' ili kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya Kwimba mkoani Mwanza.

Mbio hizo za kilomita tano, na kilomita kumi zimefanyika Jumapili Oktoba 15, 2025 katika Jiji la Mwanza na Jiji la Dar es salaam ambapo lengo ni kukusanya kiasi cha shilingi milioni 150 za kitanzania kwa ajili ya ujenzi huo.

Akizungumza jijini Mwanza wakati wa mbio hizo, Mganga Mkuu Mkoa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa amesema hatua hiyo itasaidia kuimarisha zaidi huduma za mama na mtoto hususani kwa watoto njiti na hivyo kuokoa maisha ya watoto hao.

Amesema jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali kwa kushirikiana na shirika la JHPIEGO pamoja na taasisi ya Doris Mollel zitasaidia kuimarisha upatikanaji wa huduma za watoto njiti katika Wilaya ya Kwimba huku mkakati ukiwa ni huduma hizo kupatikana kila wilaya.

Naye Mshauri Mwandamizi wa shughuli za utekelezaji wa mradi wa USAID Afya Yangu- RMNCAH, Dkt. Riziki Ponsiano amesema fedha zitakazopatikana kupitia mbio hizo zitasaidia kuanza kwa ujenzi wa jengo hilo ambalo hadi kukamilika litagharimu zaidi ya shilingi bilioni moja.

Akizungumza kwa ni baya ya Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Mohamed Mtulyakwaku amesema ujenzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya Kwimba utaondoa adha iliyopo ikiwemo kuwasafirisha umbali mrefu hadi Hospitali ya Kanda Bugando.

Katika mbio hizo, washindi wa kilomita tano na kumi wamekabidhiwa medali na vyeti kama sehemu ya kutambua ushiriki wao katika jitihada za kuokoa maisha ya mama na mtoto hususani watoto njiti.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Washiriki wakijiandaa na mbio za hisani za 'Miles For Mothers' zilizofanyika jijini Mwanza.
Mmoja wa wakimbiaji wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' akikimbiza upepo jijini Mwanza.
Washiriki wakikimbiza upepo kwenye mbio za hisani za 'Miles For Mothers' zilizofanyika jijini Mwanza.
Mmoja wa washiriki wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' akikata upepo jijini Mwanza.
Mshiriki wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' akikata upepo.
Mmoja wa washiriki wa mbio za 'Miles For Mothers' akikimbiza upepo.
Washiriki wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Washiriki wakiendelea na mbio za hisani za 'Miles For Mothers' 2023 jijini Mwanza.
Washiriki wakiendelea na mbio za hisani za 'Miles For Mothers' zilizoandaliwa na shirika la JHPIEGO kwa kushirikiana na taasisi ya Doris Mollel ili kushangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wodi ya watoto njiti katika hospitali ya Wilaya Kwimba.
Washiriki wakiendelea na mbipo za hisani za 'Miles For Mothers'.
Washirikiwa wakiwa kwenye mbio za hisani za 'Miles For Mothers' zenye lengo la kushangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wodi ya watoto njiti katika hospitali ya Wilaya Kwimba.
Washiriki wakiwa kwenye mbio za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Washiriki wakiendelea kukimbiza upepo katika mbio za hisani za 'Miles For Mothers' zilizoandaliwa na shirika la JHPIEGO kwa kushirikiana na taasisi ya Doris Molles ili kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya watoto njiti katika hospitali ya Wilaya Kwimba.
Washiriki wakiendelea kukimbiza upepo kwenye mbio za hisani za 'Miles For Mothers'.
Washiriki wakiwa kwenye mbio za hisani za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Washiriki wakiendelea kukimbiza upepo.
Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba- Mohamed Mtulyakwaku (wa tatu kushoto) akikabidhi cheti kwa washindi wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba- Mohamed Mtulyakwaku (wa tatu kushoto) akikabidhi cheti kwa mshindi wa pili wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' umbali wa kilomita tano, jijini Mwanza.
Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba- Mohamed Mtulyakwaku (wa tatu kushoto) akikabidhi cheti kwa mshindi wa kwanza wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' umbali wa kilomita tano jijini Mwanza.
Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba, Mohamed Mtulyakwaku (kushoto) akikabidhi cheti kwa mshindi wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba- Mohamed Mtulyakwaku (kushoto) akikabidhi cheti kwa mshindi wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba, Mohamed Mtulyakwaku (kushoto) akikabidhi cheti kwa mshindi wa mbio za hisani za 'Miles For Mothers' jijini Mwanza.
Picha ya pamoja.
Washindi wa mbio za kilomita tano na kilomita kumi wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi.
TAZAMA BMG TV HAPA CHINI
SOMA PIA>>> HABARI ZAIDI HAPA

No comments:

Powered by Blogger.