LIVE STREAM ADS

Header Ads

MWANZA: Wadau wajadili mitaala ya uhandisi maji na maendeleo ya jamii

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Wadau wa fani ya uhandisi na maendeleo ya jamii wakiwemo kutoka mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira jijini Mwanza (MWAUWASA), mamlaka ya maji vijijini (RUWASA), mamlaka ya taifa ya umwagiliaji, wakufunzi wa vyuo vya uhandisi na maendeleo ya jamii wamekutana Misungwi mkoani Mwanza kujadili mapitio ya mitaala ya programu ya uhandisi maji na maendeleo ya jamii.

Majadiliano hayo ya siku moja yamefanyika Alhamisi Desemba 14, 2023 katika ukumbi wa chuo cha maendeleo ya jamii ufundi Misungwi (Misungwi CDTTI).

Makamu Mkuu Taaluma wa chuo hicho, Dongo Nzori amesema lengo ni kupitia hiyo na kutoa maoni ya mwisho kabla ya kuwasilishwa katika Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kwa ajili ya kuidhinishwa.

Amesema kozi ya uhandisi maji na maendeleo ya jamii ikipitishwa na NACTVET itakuwa kozi ya pili katika vyuo vyao vya maendeleo yajamii ufundi Misungwi mkoani Mwanza na Mabughai kilichopo Lushoto mkoani Tanga ambapo itasaidia kuleta tija katika sekta ya umwagiliaji.

"Tumeamua kuleta huu mseto wa uhandisi maji na maendeleo ya jamii kwa sababu utasaidia kupunguza rasilimali watu, kuongeza ufanisi katika kusimamia miradi ya maji pamoja na kurahisisha ujenzi wa miundombinu ya maji" amesema Nzori.

Amesema kwa sasa kwenye kozi ya uhandisi ujenzi na maendeleo ya jamii ina wanafunzi zaidi ya 900 katika vyuo hivyo ambapo Misungwi kuna wanafunzi 600 na Mabughai 300 huku idadi ikitarajiwa kuongezeka baada ya kozi ya uhandisi maji na maendeleo ya majii kuanza kutolewa ambayo pia itazalisha wataalamu wanaohitajika katika soko la ajira.

Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi Mabughai wilayani Lushoto, Erasmus Hipoliti amesema mtaala wa uhandisi maji na maendeleo ya jamii utasaidia vijana wengi kupata fursa za ajira kwa namna utakavyotoa wigo wa kushiriki katika masuala ya MMaendeleo ya Jamii na uhandisi maji.

Amesema bado kuna changamoto ya miradi ya maji katika jamii ndiyo maana wameanzisha kozi hiyo ili kuandaa wataalamu watakaoibua miradi ya maji hatua itakayosaidia kutatua changamoto zilizopo.

Kwa upande wake Mhandisi Willybert Bujiku kutoka MWAUWASA Kanda ya Misungwi, amesema kozi hiyo italeta manufaa makubwa kwa Serikali ambapo akiajiriwa mtu aliyesoma uhandisi maji na maendeleo ya jamii atafanya kazi kwa ufanisi mkubwa huku pia ikiongeza wigo kwa wahandisi kufanya kazi kwa weledi zaidi.

Awali akizungumza wakati wa kufungua warsha hiyo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju ameshauri maboresho ya mitaala ya uhandisi maji na maendeleo ya jamii kusaidia kuzalisha wataalamu wenye ujuzi na weledi utakaosaoidia kuchochea maendeleo katika jamii.
Na Hellen Mtereko, Mwanza
Makamu Mkuu Taaluma Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi Misungwi CDTTI, Dongo Nzori akizungumza kwenye warsha ya wadau kujadili mitaala ya programu za uhandisi maji na maendeleo ya majii iliyofanyika katika chuo hicho.
Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi Mabughai mkoani Tanga, Erasmus Hipoliti akizungumza wakati wa warsha hiyo.
Wadau wa maji na maendeleo ya jamii wakiwa kwenye majadiliano ya mitaala ya programu ya uhandisi na maendeleo ya jamii.
Wadau wakiwa kwenye majadiliano.
Wadau wakiwa kwenye majadiliano.
Wadau wakiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Amon Mpanju (katikati waliokaa).
Wadau wakiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Amon Mpanju (katikati waliokaa).
PIA SOMA>>> HABARI ZAIDI HAPA

No comments:

Powered by Blogger.