Pamba Jiji FC yakabidhi msaada kwa wenye mahitaji maalumu
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Salala amesema hatua hiyo ni sehemu ya matendo ya huruma ikiwa ni sehemu ya matukio muhimu ya hamasa kuelekea Siku ya Pamba (Pamba Day) itakayofanyika Agosti 10,2024 CCM Kirumba.
Wakitoa shukurani baada ya kupokea mahitaji hayo, Mwalimu Rehema Kagembe na mwanafunzi
Shamim Abdallah wameiombea baraka timu ya Pamba Jiji FC wakisema hatua ya kuwakumbuka wenye mahitaji maalumu itachagiza ushindi wao kwenye ligi kuu msimu wa mwaka 2024/25.
Matukio mbalimbali yameendelea kufanyika mkoani Mwanza ikiwemo uzinduzi wa mashina ya mashabiki wa Pamba Jiji FC, kuuza tiketi na jezi kuendelea kilele cha 'Pamba Day' Agosti 10, 2024 uwanja wa CCM Kirumba.
Pamba Jiji FC wanasema 'Mbele, Mbele Yao Zaidi' na 'Utakpigwa Kama Utakavyokuja'.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
No comments: