LIVE STREAM ADS

Header Ads

Rais Samia asaka fursa zaidi Afrika Kusini

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamua kusaka fursa zaidi za kiuchumi nchini Afrika Kusini kwa ajili ya wananchi wake wa Tanzania.

Ili kulifanikisha hilo Rais Dkt. Samia amekutana na Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa kabla ya kuanza kwa mkutano wa G20 unaofanyika nchini Brazil.

Viongozi hao walishiriki katika mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili na kutafuta njia za kuendeleza masuala yenye maslahi kwa pande zote mbili.

Afrika Kusini na Tanzania zina ushirikiano mkubwa wa kihistoria, unaoimarishwa zaidi na uhusiano muhimu wa kiuchumi.

Afrika Kusini imeibuka kuwa mmoja wa washirika wa msingi wa kibiashara wa Tanzania ndani ya kanda ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).

Biashara kati ya mataifa hayo mawili imeshuhudia ukuaji mkubwa, ambapo Afrika Kusini iliuza bidhaa zenye thamani ya bilioni 9.8 kwa Tanzania mwaka 2023, kutoka bilioni 8.8 mwaka 2022.

Ongezeko hili la kasi linaonyesha kuimarika kwa uhusiano wa kiuchumi, na kusisitiza uwezekano wa ushirikiano zaidi katika maeneo ya biashara, uwekezaji na maendeleo ya kikanda.

Mkutano kati ya Marais hao ni dhihirisho la urafiki wa kudumu na ushirikiano wa kimkakati kati ya Afrika Kusini na Tanzania ndani ya mfumo mpana wa SADC na majukwaa ya kimataifa.
#KaziInaongea

No comments:

Powered by Blogger.