LIVE STREAM ADS

Header Ads

Bilioni 114 zafanikisha mradi wa maji Manyara

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Katika kuendelea na kampeni yake ya kutokemeza tatizo la maji nchini, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan
imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 114 kwa ajira ya kufikisha maji kwa wananchi mkoani Manyara.

Kiasi hicho cha fedha kimetolewa ikiwa ni kutekeleza kampeni ya kuondoa tatizo la maji nchini.

Mafanikio hayo ya miradi ya maji, yameweza kuwafikia Wananchi waliokuwa wanakabiliwa na uhaba wa maji mkoani Manyara.

Miongoni mwa fedha hizo, Shilingi bilioni 89.7 zilitolewa kwa ajili ya miradi ya maji vijijini, shilingi bilioni 24.4 kwa ajili ya miradi ya maji mijini.

Katika kipindi cha miaka mitatu, Serikali kupitia mradi wa mfuko wa maji (NWF), imewezesha maeneo yaliyokuwa yanakabiliwa na uhaba wa maji, kuweza kupata huduma hiyo.
#KaziInaongea

No comments:

Powered by Blogger.