BOMOA BOMOA KATIKA MTAA WA MAKOROBOI JIJINI MWANZA YASABABISHA TAHARUKI KWA TAKRIBANI MASAA MANNE. MSIKITI WA WAHINDI NUSRA UCHOMWE MOTO. SOMA NA TAZAMA KILICHOJILI.
![]() |
Nusra Msikiti huu uungue kwa moto, baada ya mbao zilizokuwa zimewekwa eneo hili kuchomwa moto na baadhi ya vijana ambao walikuwa wanapinga kuondolewa katika eneo hili la Makoroboi. |
![]() |
Hili ni eneo ambalo bomoa bomoa imefanyika ambalo liko katika Mtaa wa Makoroboi Jijini Mwanza. Eneo hili kulia na kushoto kulikuwa na vibanda vya wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama machinga. |
![]() |
Mbao zilizobomolewa kabla ya kuchomwa moto na baadhi ya machinga |
![]() |
Barabara ya kuingia na kutoka eneo la Msikiti wa Wahindi katikati ya Mtaa wa Makoroboi mara baada ya bomoa bomoa. |
![]() |
Ndivyo ilivyokuwa wakati wa zoezi la ubomoaji wa vibanda vya wafanyabiashara ambao wanafanyia biashara zao eneo ambalo inadaiwa kuwa haliruhusiwi kwa ajili ya biashara. |
Maaskari wa kutuliza ghasia FFU walikuwa bado wakiendelea na juhudi za kutuliza ghasia ambazo zilikuwa zimeanza kufanywa na baadhi ya machinga katika Mtaa wa Makoroboi ambako alfajiri ya leo imefanyika bomoa bomoa.
"Sisi tunashangaa kwanini wanakuja kutubomolea mabanda yetu ya kufanyia biashara tena bila taarifa, ni bora wangetupa taarifa. Tuna watoto tunasomesha sasa tutawasomeshaje? hapa nilipo kama mimi sijui nitafanyaje, jana nimechukua mkopo bank na nategemea biashara hii ndogo ndogo kwa ajili ya kurejesha huo mkopo, sasa walivyotubomolewa wanategemea nini, hatukubali hatukubali kamwe..." Alisema mmoja wa machinga ambe alikumbwa na bomoa bomoa hiyo.
Baada ya bomoa bomoa hiyo kufanyika alfajiri ya hii leo, machinga walioko Makoroboi walianza kufanya fujo na hivyo kusababisha shughuli zote katikati ya jiji la Mwanza kusimama hadi hivi sasa majira ya saa saba za mchana, huku jeshi la polisi likitumia zaidi ya masaa matatu kupambana na machinga hao kwa kutumia mabomu ya kutoa machozi.
"Mimi nawaomba hawa vijana wajaribu kuwa watulivu, hili suala tutakaa na viongozi wao tutazungumza ili tuone namna ya kufanya ili tuhakikishe hawa vijana wanatafuta riziki, mimi nilisikia kutoka kwa Mkuu wa Mkoa kwamba chanzo ni wahindi wanalalamika kwa hiyo mimi kama mlezi nitaenda nipige magoti kwa wahindi kwamba hakuna njia mwafanya ya kufanya ili vijana waendelee kutafuta riziki, kwa hiyo majibu nitayapata kutoka kwa wahindi, hakuna kinachoshindikana kwa hiyo nawaomba vijana wawe watulivu" Alisema Mlezi wa Machinga Mkoa wa Mwanza Alfred Wambura mara baara ya bomoa bomoa hiyo, zikiwa ni dakika chache kabla ya kuibuka kwa taharuki katika Mtaa wa Makoroboi.
Mpaka sasa hakuna mamlaka yoyote ambayo imetoa taarifa sahihi juu ya usahihi wa kuwepo machinga katika mtaa huo wa Msikiti wa Wahindi uliopo Makoroboi ama laa, japo machinga walioko katika eneo hilo wanasema wao kufanyia biashara mkabara na msikiti huo hakuoathiri chochote.Viongozi wa Machinga hawakuweza kupatikana hata baada ya kupigiwa simu zilikuwa hazipokelewi ili kutoa ufafanuzi juu ya suala hii, huku pia juhudi za kuwatafuta viongozi wa halmashauri ya jiji la Mwanza nazo zikigonga mwamba kwa madai kwamba wako nje ya ofisi kwa ajili ya vikao vya dharura. Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza Valentino Mlowola hakuweza kuzungumzia operation hiyo kwa madai kuwa yuko Jijini Dar es salaam.
No comments: