TAARIFA KAMILI KUHUSIANA NA MCHAWI ALIEDONDOKA KATIKA HOSPITAL YA MKOA WA MWANZA SEKOUR TOURE, NI BAADA YA KUGOMBANA NA WENZAKE WANNE AKIWEMO MAMA MCHUNGAJI.
![]() |
Anaesadikiwa kuwa mtalaamu wa anga/mchawi.....(Picha Y.Kagenzi) |
Duru za habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa mwanamke huyo alidondoka maeneo hayo baada ya kutokea kutokuelewana na wenzake wane aliokuwa nao, akiwemo mama mmoja ambae mwanamke huyo amemtaja kuwa ni Mama Mchungaji wa kanisa la...(Jina linahifadhiwa).
Mwanamke
huyo amekutwa maeneo hayo akiwa na Taulo kiunoni ambapo katika kujitetea kwake
amekiri kuwa yeye ni mchawi na amedondoka katika maeneo hayo baada ya kutokea
ugomvi akiwa na wenzake ambao walimzidi nguvu na kumpelekea yeye adondoke chini.
“Kwa maelezo
niliyopewa alikamatwa (kitalaamu) wakati akienda kuwachukua watoto wadogo kwenye hospital
hiyo (Sekour Toure) akawa amenaswa na kushindwa kuendelea na kazi yake ya uchawi” Aliieleza Mtanzania
Media mmoja wa wananchi wa Jiji la Mwanza waliokuwa wakifuatilia tukio hilo kwa makini kabisa.
Taarifa za
kudondoka kwa mwanamke huyo zimewaacha vinywa wazi watu waliokuwepo eneo la tukio, huku baadhi yao wakishindwa kutoa maelezo ya kina kuhusiana na tukio hilo
ambapo baadhi yao wameamini kuwa mwanamke huyo ni mchawi kweli huku wengine
wakishindwa kuamini na kudhania labda ni mtu tu ambae hana makazi maalumu na
amekutwa maeneo hayo akiwa amejihifadhi.
No comments: