LIVE STREAM ADS

Header Ads

ASKARI WA USALAMA BARABARANI MKOANI MWANZA WALALAMIKIWA. MADUDU WANAYOFANYA YAANIKWA WAZI.

Dereva Akielezea Kero anazozipata kutoka kwa Maaskari wa Usalama Barabani Mkoani Mwanza.
Baadhi ya Askari wa Usalama Barabarani Mkoani Mwanza Wamelalamikiwa na Madereva wa daladala, Kutokana na tabia ya kuwabambikizia makosa na Kuwatoza faini kinyume cha Sheria, ikiwa ni pamoja na Kuanzisha utaratibu wa Kuwatoza Madereva fedha Kiasi cha Shilingi 5,000 kila siku ili daladala zao zisikaguliwe.


Madereva walioelezea Kukerwa na Tabia za baadhi ya Askari hao ni wale wanaofanya Safari zao Kuanzia Nyegezi, Buhongwa Wilayani Nyamagana kwenda Ishokera, Misasi, Sarawe hadi Wilayani Misungwi ambapo wamebainisha kuwa Maaskari wa Usalama barabarani katika maeneo hayo wamekuwa na Utendaji kazi Mbovu ambao hauzingatii sheria na kanuni zinazowaongoza.

Dereva Akielezea Kero anazozipata kutoka kwa Maaskari wa Usalama Barabani Mkoani Mwanza.
Wakitoa Malalamiko hayo hii leo katika Vituo vyao vya kazi vilivyopo Buhongwa na Nyegezi Wilayani Nyamagana, Madereva hao wameeleza kuwa baadhi ya Maaskari wa Usalama barabara katika Barabara ya Misungwi wamekuwa na tabia ya kuwabambikizia makosa na kuwatoza faini kinyume na taratibu.



Aidha wamebainisha kuwa Maaskari hayo wameanzisha utaratibu wa Kuwatoza shilingi Elfu Tano (5,000) kila siku kwa madai ya magari yao kutokukaguliwa na ikiwa dereva atakaa kutoa kiasi hicho hutafutiwa kosa lolote na hatimae kutozwa faini ambayo hufikia hadi shilingi Elfu Thelathini (30,000).

Dereva Akielezea Kero anazozipata kutoka kwa Maaskari wa Usalama Barabani Mkoani Mwanza.

“Hawa maaskari wanapokezana kusimamisha Magari na kututafutia makosa. Ukionekana kuwasumbua unaambiwa siku hizi umekuwa mjanja hutaki kujiunga na sisi. Kujiunga kwenyewe unaambiwa utoe shilingi Elfu tano kila siku ili gari lako lisikagulie na ukikataa kama huna kosa wanakuacha unaondoka na wanapiga simu unakamatwa kwa mbele unaambiwa unaendesha gari kwa Speed (mwendo Kasi) na unaandikiwa faini” Alieleza mmoja wa Madereva hao ambae anafanya safari zake za Nyegezi, Misungwi, Misasi na Sarawe.


“Tabia hii ya Kutoa Shilingi Elfu Tano kila Siku ambayo wenyewe wanaiita Cheka Time imekuwa ni Suala endelevu. Binafsi sijafurahia vitendo wanavyovifanya” Alieleza dereva mwingine ambae yeye anafanya safari zake za Buhongwa Wilayani Nyamagana kwenda Misasi Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Dereva Akielezea Kero anazozipata kutoka kwa Maaskari wa Usalama Barabani Mkoani Mwanza.
 Akizungumzia kero zilizotewa na Madereva hao, Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa (Victoria Drivers Assosiation) Dede Petro Dede ameeleza kuwa kero zote zilizotolewa na madereva hao zinafanyiwa kazi na tayari viongozi wa chama hicho sanjari na baadhi ya madereva wamekutana na Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani Mkoani Mwanza ili kujadili namna ya kuondoa kero hizo kwa madereva.


“Hizi kero zinafanyiwa kazi. Kesho (Alhamisi) Madereva hawa walikuwa wamepanga kugoma, lakini sisi kama uongozi tukasema hapana haiwezekani wananchi (abiria) wapate shida ya usafiri kwa sababu ya watu wachache. Kwa hiyo tumekutana na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabari na tumezungumzia suala hili na tutakutana tena katika kikao cha pili kwa ajili ya kuhakikisha kero hizi zinaondolewa na madereva wanafanya shughuli zao kwa mjibu wa sheria na taratibu” Alisema Dede na kuongeza...


“Kila siku kukamatwa. Usipojiunga kutoa elfu tano unakamatwa na kuambiwa utoe shilingi elfu thelathini. Huu ni ujanja wa baadhi ya watu kutaka kuichafua Serikali. Tunaomba hii Serikali sikivu iwaangalie hawa Maaskari. Kwanza wamekaa katika hii barabara ya Misungwi kwa muda mrefu, wabadilishwe maana wamezoeleka…”
 


Dereva Akielezea Kero anazozipata kutoka kwa Maaskari wa Usalama Barabani Mkoani Mwanza.

Akizungumzia kero zinazolalamikiwa na Madereva hao katika Kipindin cha Metro Evening Drive Kinachorushwa na Metro FM Jijini Mwanza, Dede alieleza kuwa kitendo cha maaskari wa usalama barabarani kupokea pesa kutoka kwa madereva ili magari yao yasikaguliwe ni hatari kwa kuwa kuna baadhi ya madereva hawana leseni hivyo wanaweza kuwa wanatoa pesa na kubeba abiria jambo ambalo linahatarisha usalama wa abiria.

Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa Dede Petro Dede akizungumza na Madereva baada ya kueleza kero zao katika eneo la Nyegezi.
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa Dede Petro Dede akizungumza na Madereva baada ya kueleza kero zao katika eneo la Buhongwa.
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa Dede Petro Dede akizungumza na Madereva baada ya kueleza kero zao katika eneo la Buhongwa.
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa Dede Petro Dede akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini Kwake.


Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa Dede Petro Dede akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini Kwake.
Mtanzania Media, Juhudi za Kumtafuta Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Mwanza ili kuzungumzia sula hili bado zinaendelea.
Na: George Binagi @Radio Metro & Mtanzania Media

No comments:

Powered by Blogger.