LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAFARIKI KWA KUFUKIWA NA MAWE WAKITAFUTA RUPIA ZILIZOACHWA NA WAKOLONI MKOANI MWANZA.

Shimo ndilo hili
Watu wawili wamepoteza Maisha Mkoani Mwanza baada ya Kukosa hewa katika Miamba wakitafuta Rupia katika Mtaa wa Kangaye B Wilayani Ilemela, ambapo Mwili wa Mtu Mmoja kati ya wawili hao umeshindwa kupatikana kutokana na mazingira magumu yaliyoko katika eneo hilo.


Tukio hilo lilitokea Jaza asubuhi (Jumatano) ambapo hadi kufikia jana Mwili wa Mtu mmoja alietambulika kwa jina la Zubery Kaima (45) ulishindwa kupatikana mara baada ya juhudi za wananchi na Serikali ya Wilaya ya Ilemela kushindikana kutokana na Kukwamishwa na Miamba iliyozunguka katika eneo hilo la tukio.


Akizungumzia Tukio hilo, Bi.Zuwena Khamis ambae mme wake alipoteza maisha katika tukio hilo ameeleza kuwa alipokea taarifa za watu kufukiwa na miamba katika eneo hilo la Kangae B na alipofika katika eneo hilo alikuta tayari mmewe Sufian Khamis amekwisha poteza maisha.(Mwili wa Sufiani ulifanikiwa kufukuliwa siku ya jana).


Wakizungumzia Tukio hilo baadhi ya wananchi wa Mtaa huo wa Kangaye B wamesema Kuwa chanzo cha Tukio hilo ni Imani Potofu ambapo walidai kuwa mmoja wa hao waliopeza maisha alidai Kuoteshwa na Mungu kuwa eneo hilo lina mali ambazo ziliachwa na Wakoloni wa Kijerumani.


Wananchi wakiwa katika eneo la Tukio.
Kwa Upande wake Sultan Said ambae ni Mmoja wa Watu waliongia katika Mashimo ya Miamba hiyo kwa ajili ya Kujaribu kuutafuta mwili wa Sufian Khamis ambae juhudi za kuutafuta mwili wake zilishindikana, alisema kuwa walishindwa kuupata mwili huo kutokana na kuwa katika Miamba Miamba ya Mawe yenye Upenyo mdogo usioweza kuruhusu binadamu kuingia huku akiongeza kuwa pamoja na jitihada kubwa walizotumia wakiwa na Tochi kuutafuta mwili huo lakini bado hawakuuona mwili huo.


Akizungumzia Tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Amina Masenza aliwataka Wakazi na wananchi wa eneo hilo kuacha kuamini mambo ya kufikirika na yasiyo ya kweli ambayo yanaweza kuleta hatari katika maisha ya binadamu na hivyo kuwasihi kuwa ni vyema wawe wepesi wa kutoa taarifa katika mamlaka husika pale wanapoona vitendo visivyo vya kawaida katika jamii.


Tukio hilo la Kusikitisha lilitokea Juzi asubuhi mara baada ya Watu hao kuingia katika Shimo hilo lenye Miamba katika eneo la Kangaye B Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza kwa lengo la Kufuatilia MALI ambazo zimeelezwa kuwa Ziliachwa na Wakoloni wa Kijerumani katika Mashimo yaliyo katika eneo hilo.

NA: HALITH JAHA ALLY.

No comments:

Powered by Blogger.