Waziri wa Ujenzi Mh.Dk.John Pombe John Magufuli.
Waziri
wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuli leo amezindua Kivuko Kipya Jijini Mwanza,
ambacho kitakuwa Kikifanya Safari zake katika Mwambao wa Ziwa Victoria kwa
lengo la Kupunguza adha ya Usafiri kwa wananchi kutokana na Msongamano wa
Magari katikati ya Jiji.
Kivuko hicho ambacho kimepewa jina la MV.TEMESA kimegharimu fedha za
Kitanzania zaidi ya Shilingi Milioni 640 kitakuwa Kikifanya Safari zake Kuanzia
Eneo la Sweya kupitia Butimba TCC, Mkuyuni, Igogo hadi Kirumba huku Matarajio
ya baadae yakiwa ni kuongeza safari za kivuko hicho Igombe na Kayenze.
|
No comments: