Washiriki wa Mkutano wa Vijana Mkoani Mwanza ikiwa ni sehemu ya Kuadhimisha siku ya dadi ya Watu Duniani inayotarajiwa Kuadhimishwa Kesho July 11. Mkutano huu umefanyika kwa Ushirikiano Mkubwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu duniani (UNFPA) na Wadau wengine kama Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini ( RITA) chini ya Uratibu wa Ofisi ya Rais Tume ya Mipango.
Imeelezwa kuwa ili kupata Mafanikio yanayotokana na Uwekezaji kwa
Vijana, ni mhimu kuwa na Mpango Mkakati unaolenga Kuwekeza kwa Vijana katika
Maeneo yenye Umuhimu kwa Vijana.
Hayo yameelezwa hii leo Mkoani Mwanza na Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya
Nyamagana Marcella Mayala kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, wakati akifungua
Mkutano wa Vijana ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu
Duniani ambayo inatarajiwa kuadhimishwa Kesho Mkoani Mwanza.
|
No comments: