Katika hatua
nyingine Ndasa pia aliwakumbusha wananchi kwamba
mchakato wa Katiba bado unaendelea, na umefikia hatua za mwisho ambazo zinahitaji
ushiriki wa kila mmoja hivyo ni vyema wakatambua kwamba mchakato huo wa
Katiba ukipita sasa, Katiba itakayopatikana itatumika kwa hivi sasa na
baadae kwa vizazi vingi vijavyo, na itachukua muda mrefu sana kabla ya
kutungwa Katiba nyingine hivyo akawataka kujitokeza kwa wingi katika kushiriki
zoezi la upigaji kura pindi rasimu ya tatu itakapowasilishwa kwao.
Asilimia kubwa ya wadau
waliojitekeza katika Uzinduzi wa Kampeni hiyo, walikuwa wakivutana mara kwa
mara kuhusiana na mwendendo wa katiba mpya unavyoendelea hivi sasa, ambapo
mvutano huo uligawanyika katika makundi mawili, kundi la kwanza likionekana
kukubaliana na mchakato unavyoendelea mpaka hivi sasa, huku kundi jingine
likionyesha kutoridhishwa kabisa na mchakato huo na kuonyesha wazi wazi kutaka
bunge maalumu la katiba linaloendelea mjini Dodoma kuahirishwa badala ya
kuendelea kugharibu pesa za watanzania.
|
No comments: