LIVE STREAM ADS

Header Ads

MARIE STOPES TANZANIA YAFUNGUA ZAHANATI NYEGEZI JIJINI MWANZA.

Kikundi cha Ngoma Asilia kutoka Bujora Mkoani Mwanza kikitumbuiza katika Ufunguzi huo. Na huu ni mchezo wa Kucheza na Nyoka. Read More kujionea kilichojili.
Vijana na Jamii nzima kwa ujumla wameshauriwa kuzingatia mfumo wa njia za Uzazi wa Mpango katika kupanga familia, kwa kuwa mfumo huo utawawezesha wanafalia kupanga familia watakayoweza kuihudumia sanjari na vijana kufikia malengo yao.


Ushauri huo ulitolewa hii jana Mkoani Mwanza na Elly Rewete ambae ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala kutoka Marie Stopes Tanzania, katika Uzinduzi wa Kitua cha Afya cha Marie Stopes kilichopo Nyegezi Wilayani Nyamagana.


Rewete ambae alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Marie Stopes katika Uzinduzi huo, alibainisha kuwa Uzazi wa Mpango ndiyo njia pekee inayoweza kuondoa vikwazo vya Mimba zisizotarajiwa, Kufikia Malengo kielimu pamoja na kupambana na umasikini na hatimae kuchangia katika pato la Taifa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Valentino Francis Bangi akiwa tayari kabisa kwa ajili ya kukata Utepe kama ishara ya ufunguzi wa Kituo hicho cha Afya cha Marie Stopes Nyegezi.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Valentino Francis Bangi akikata Utepe kama ishara ya ufunguzi wa Kituo hicho cha Afya cha Marie Stopes Nyegezi Jijini Mwanza.
Akizungumza kwa niaba ya Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mganga Mkuu wa Mkoa Mwanza Valentino Francis Bangi alitoa rai kwa wanafamilia wote kushiriki katika njia za Uzazi wa Mpango badala ya suala hilo kuachiwa wanawake pekee.

Aidha alisisitiza kwamba makundi yote yanayostahili kupata huduma za Afya bure katika jamii, yanapaswa kutambuliwa ambapo zaidi amesisitiza kundi la wazee walio na umri wa miaka 60 na kuendelea kuandikishwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu bila malipo kupitia huduma ya tiba kwa kadi.



Baada ya agizo hilo, Diwani wa Kata ya Butimba Masunu Dismas Masunu akabainisha kwamba Kata ya Butimba na Jiji la Mwanza kwa ujumla imekwisha anza utekelezaji wa kuhakikisha kwamba wazee wote wanatibiwa bure, ambapo jumla ya wazee 902 wamekwisha pewa vitambulisha vya matibabu ya bure ambapo katika Kata ya Butimba Wazee takribani 113 tayari wamepewa vitambulisho hivyo.



Nao baadhi ya wananchi hususani vijana waliofika katika uzinduzi wa kituo hicho cha Marie Stope kilichopo Nyegezi Wilayani Nyamagana, walieleeza kwamba suala la Uzazi wa Mpango bado halijaeleweka sana katika jamii hivyo ni vyema elimu zaidi ikazidi kutolewa kwa vijana na wananchi wote kwa ujumla ili kuwaongezea uelewa zaidi kuhusiana na masuala ya uzazi wa mpango.


Elly Rewete ambae ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala kutoka Marie Stopes Tanzania (Kushoto), akifuatiwa na Miss Tanzania Happness Watimanywa (Katikati) na wa mwisho (kulia) ni Miss Marie Stopes Narietha Boniphace.
Miss Tanzania Happness Watimanywa (Kushoto) akiwa na Miss Marie Stopes Narietha Boniphace (Kulia). Wote ni Mabalozi wa Marie Stopes ambao wanahamasisha vijana na wanajamii kwa ujumla kuzingatia njia za uzazi wa mpango.
Wananchi waliofika katika uzinduzi huo.
Kuanzia Agost 25 hadi jana Agost 29 Huduma mbalimbali za Uzazi wa Mpango zilitolewa bure kwa wananchi kama sehemu ya Ufunguzi wa Kituo hicho. Huduma zilizotolewa ni pamoja na Kufunga Uzazi kwa akina mama, akina baba, kuweka kitanzi, kipandikizi na sanjari na huduma nyinginezo zote za uzazi mpango.
Miss Tanzania Happness Watimanywa.
Miss Tanzania Happness Watimanywa
Elly Rewete ambae ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala kutoka Marie Stopes Tanzania.

Diwani wa Kata ya Butimba Jijini Mwanza Masunu Dismas Masunu.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Valentino Francis Bangi.
Mwanahabari kutoka Kwa Neema Radio Joel Maduka (Katikati) akiwa na Miss Tanzania Happness Watimanywa (Kushoto) pamoja na Miss Marie Stopes Narietha Boniphace (Kulia).
Mkurugenzi wa Mtanzania Media na Mwanahabari kutoka Radio Metro George Binagi (Katikati) akiwa na Miss Tanzania Happness Watimanywa (Kushoto) pamoja na Miss Marie Stopes Narietha Boniphace (Kulia).
Miss Tanzania Happness Watimanywa (Kushoto) akiwa na Miss Marie Stopes Narietha Boniphace (Kulia). Wote ni Mabalozi wa Marie Stopes ambao wanahamasisha vijana na wanajamii kwa ujumla kuzingatia njia za uzazi wa mpango.
Na: George Binagi @99.4 Metro FM & Mtanzania Media.

No comments:

Powered by Blogger.