LIVE STREAM ADS

Header Ads

ZAWADI MISS LAKE ZONE 2014 HADHARANI. WAREMBO WAJINADI.



Zawadi za Washindi wa Shindano laMiss Lake Zone 2014 linalotarajiwa kufanyika hii leo jumamosi Agost 30 katika Uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza tayari zimewekwa hadharani.

Flora Lauwo ambae ni muandaaji wa Shindano hilo kupitia kampuni yake ya Flora Promotion amebainisha kuwa,
Mshindi wa Kwanza atapata zawadi ya gari yenye thamani ya shilingi Milioni Kumi, Mshindi wa Pili atajipatia zawadi Bajaji yenye tahamani ya shilingi milioni nne, ambapo mshindi wa tatu atapata fursa ya kusomeshwa huku mrembo mwenye kipaji akijishindia zawadi ya pikipiki yenye thamani ya shilingi Milioni moja na laki sita sanjari na zawadi mbalimbali kutoka kwa wadhamni.


Kwa upande wake Benny Mwangi ambae ni Meneja wa Lenny Hotel iliyopo Mkoani Geita, ameeleza kuwa Lenny Hotel ilijitokeza kudhamini shindano hilo kwa lengo la kuboresha mashindano hayo, huku akiongeza kuwa jamii inapaswa kubadili mtizamo na kuachana na fikra potofu kuwa mashindano ya urembo ni uhuni. Lenny Hotel katika udhamini wake imetoa zawadi ya gari yenye thamani ya shilingi Milioni kumi kwa ajili ya mshindi wa kwanza.

Nao Washiriki wa Shindano hilo wameelezea furaha yao baada ya kuchaguliwa kuiwakilisha Mikoa yao ya Kanda ya Ziwa, ambapo kila Mkoa umetoa Washiriki watatu kwa ajili ya kujishiriki Shindano hilo la Miss Lake Zone 2014 ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni shilingi 5,000, 10,000 na 30,000.

Kila Mmoja wa washiriki hao amejigamba kuibuka mshindi wa kwanza na hivyo  kuondoka na zawadi ya gari ambapo wamewasihi wakazi wa Kanda ya Ziwa ikiwemo Mkoa wa Mwanza kujitokeze kwa wingi hii leo katika Uwanja wa CCMK Kirumba ili kushuhudia shindano hilo la Miss Lake Zone 2014.





"Mtoto Mtoto"

Funguo za Gari kwa ajili ya Mshindi wa Kwanza wa Miss Lake Zone 2014.

Judith Josephat Maturege (Kulia) ambae ni Matron wa Mamiss wanaoshiriki shindano hilo akishow love na mdau.
"Matron bwana alitokea kuvutiwa na Pen yangu...ikabidi nimuachie"

Benny Mwangi ambae ni Meneja wa Lenny Hotel iliyopo Mkoani Geita.

Benny Mwangi ambae ni Meneja wa Lenny Hotel iliyopo Mkoani Geita akiwa katika mahojiano na Wanahabari.

Wadau wakichukua kumbukumbu.

Zawadi za Washindi wa Miss Lake Zone 2014.


Watoto wanapendeza kiukweli. Hutakiwi kukosa leo katika Uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza. Jukwaani atakuwepo Barnaba Boy pamoja na SkyLite Band.
Na: George Binago @99.4 Metro FM & Mtanzania Media.

No comments:

Powered by Blogger.