Asia Kapande ambae ni Mwenyekiti wa Bodi wa Shule za Green View (Kulia) Akilishwa Keki Mgeni Rasmi Kaimu
Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Rufaa Bugando Profesa Dr.William Mahalu (Kushoto).
Aidha
aliongeza kuwa, awali kabla ya Kuanzishwa kwa shule za Green View wazazi wengi
walikuwa na hurka ya kuwapeleka watoto wao kusoma nje ya nchi, jambo ambalo kwa
sasa halipo tena baada ya Shule za Green View kuanzishwa kutokana na elimu bora
inayotolewa na Shule hizo ambazo zinatumia mitaala ya kiingereza kufundishia.
Akizungumzia
mafanikio ya Shule za Green View, Matemba alibainisha kwamba kwa miaka
takribani yote, wanafunzi wake wamekuwa wakifaulu katika mitihani yao huku
akiitolea mfano mitihani ya kitaifa ya kidato cha nne na darasa la saba ya
mwaka jana kwamba wanafunzi wote wa shule za Green View waliweza kufaulu
mitihani yao.
|
No comments: