JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA LAPIGA MARUFUKU MAANDAMANO YA CHADEMA.
Kesho, yakiwa na lengo la kupinga kuendelea kwa Vikao vya Bunge Maalimu la Katiba linaloelekea Ukingoni Mjini Dodoma.
Kauli ya
Jeshi hilo imetolewa hii leo na Kamanada wa Polisi Mkoa wa Mwanza
SACP.Valentino Mlowola, ikiwa ni dakika chache baada ya Uongozi wa Chadema Mkoa
wa Mwanza Kutangaza kufanya Maandamano hayo.
Kamanda Mlowola
amesema kuwa Jeshi la Polisi limepiga marufuku maandamano yanayohusiana na
Bunge Maalumu la Katiba, kwa kuwa Bunge hilo linaendeshwa kwa mjibu wa Kanuni
na Taratibu za Kisheria hivyo jeshi hilo haliwezi kuruhusu maandamano ambayo
yanaweza kukwamisha shughuli za maendelo.
Mbali na
hayo Kamanda Mlowola amesema kuwa kwa hivi sasa kuna shughuli za Kitaifa zinaendelea
Mkoani Mwanza ambazo ni pamoja na shughuli za Mbio za Mbwenge sanjari na Ujio
wa Makamu wa Rais, hivyo jeshi hilo haliwezi kutoa kibari kwa ajili ya Maandamano
hayo kutokana na shughuli hizo.
Kamanda wa Polisi (M) wa Mwanza SACP.Valentino Mlowola. |
Amesema
Jeshi la Polisi litahakikisha linatumia nguvu zote kwa mjibu wa Kanuni na taratibu
za Kisheria ili kuhakikisha kwamba maandamano hayo hayafanyiki, kwa lengo la
kulinda amani ya Mkoa wa Mwanza ambayo kwa hivi sasa imetawala Mkoani Mwanza,
kwa kuwa maandamano hayo yana lengo la kuvuruga amani hiyo.
Aidha Kamanda
Mlowola ametoa onyo kali kwa Uongozi wa Chadema kutofuata mkumbo wa kutaka
kufanya jambo ambalo litahatarisha amani kwa wananchi ambao ndio wapiga kura
wao, huku akiwatahadharisha Waandishi wa habari kuwa makini na maandamano hayo
katika utekelezaji wa shughuli zao kwa kuwa jeshi la polisi haliwazui watu
kufanya shughuli zao isipokuwa linawazuia watu kujihusisha na maandamano.
Kufuatia kauli hiyo ya Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza, wananchi nao
wamekuwa na maoni tofauti ambapo baadhi yao wameonekana kutounga mkono uwepo wa
Maandamano hayo kwa madai kwamba maandamano hayajengi badala yake yanaweza
kuhatarisha suala la amani huku wengine wakiyaunga Mkono maandamano hayo japo
kwa hoja ya kwamba wako tayari kuandamana endapo kama viongozi wa Chadema nao
watakuwa mstari wa mbele katika maandamano hayo.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mwanza kupitia
kwa Mwenyekiti wake Adrian Tizeba, hii leo kimetangaza kufanya maandamano siku
ya Kesho Mkoani Mwanza kwa lengo la kupinga Bunge Maalumu la Katiba ambalo
zimesalia siku chache kuhitimisha shughuli zake Mjini Dodoma, huku taarifa hiyo
ikishindwa kuweka bayana maandamano hayo yataanzia wapi wala kuhitishiwa wapi
hadi siku ya kesho ambapo suala hilo litawekwa wazi.
Wanahabari nao walipata fursa ya kuuliza Maswali, ambapo swali kubwa lilikuwa ni namna jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza lilivyojipanga katika kuwakakikishia usalama waandishi wa Habari.
|
Waandishi wa Habari hii leo wakiwa katika ukumbi wa Mikutano uliopo katika Ofisi za Kamanda Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza. |
No comments: