MAMLAKA YA HALI YA HEWA YATOA TAHADHARI KWA WANANCHI MKOANI MWANZA.
Taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo kwa vyombo vya habari imebainisha kwamba, mvua hizo
zinatarajiwa kuwa za juu ya wastani ambapo Viwango vya uhakika kwa Mkoa wa Mwanza kupata mvua za juu ya wastani ni asilimia 45, mvua za wastani asilimia 30 na za chini ya wastani asilimia 25.
zinatarajiwa kuwa za juu ya wastani ambapo Viwango vya uhakika kwa Mkoa wa Mwanza kupata mvua za juu ya wastani ni asilimia 45, mvua za wastani asilimia 30 na za chini ya wastani asilimia 25.
Kutokana na ongezeko hilo la wastani wa Mvua, Mamlaka hiyo imesema
kuwa Mvua zinatarajiwa kuwa za kutosha kwa kilimo, malisho ya mifugo, na kuongeza
chakula cha samaki katika ziwa Viktoria huku Mtiririko wa maji katika mito ukitarajiwa
kuongezeka katika maeneo mengi ya Mkoa wa Mwanza.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Vipindi vya mvua kubwa
vinavyoambatana na upepo mkali vinaweza kuongeza matukio ya mafuriko,
mmomonyoko wa udongo na kusabababisha vifo sanjari na uharibifu wa mali na
miundombinu ya mawasiliano.
Aidha taarifa hiyo imebainisha kwamba Milipuko ya magonjwa
yanayosababishwa na kutuama kwa maji na utiririshaji wa maji taka usiodhibitiwa
hususan maeneo ya mjini inaweza kujitokeza.
Mwelekeo wa mvua uliotolewa na Mamlaka hiyo umezingatia zaidi
kipindi cha msimu cha miezi mitatu ya kuanzia mwezi Agost hadi Desemba ambapo Watumiaji
wa taarifa za utabiri wa hali ya hewa wameshauriwa pia kufuatilia tabiri za saa
24, siku 10 pamoja na mwezi kama zinavyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa
nchini.
Na: George Binagi
No comments: