Yambesi
alisema miongoni mwa mafanikio yanayoonekana Serikalini yanachangiwa na Taasisi
mbalimbali kwa ushirikiano wa pamoja na Serikali, ambapo aliyataja mafanikio
hayo kuwa ni pamoja na Ujenzi na uendeshaji wa Shule za Msingi, Sekondari, Vyuo,
Vituo vya Afya pamoja na Zahanati ikiwa ni miongoni mwa mafanikio mengine mengi
yanayochagizwa na Taasisi hizo hapa nchini.
Aidha
aliongeza kuwa Serikali kupitia mpango wa ushirikishwaji wa Sekta binafsi,
imeweka kipaumbele cha kushirikiana na Taasisi mbalimbali hapa nchini kwa lengo
la kuleta maendeleo kwa jamii ya wananchi wa Watanzania, huku akiongeza kuwa
nchi itaweza kupiga hatua kubwa na kwa haraka zaidi iwapo kama wadau wote wa
maendeleo wa ndani watashirikiana na Serikali.
|
No comments: