SHIRIKA LA STARKEY HEARING LATOA AHUENI KWA WATU WENYE MATATIZO YA KUSIKIA JIJINI MWANZA.
Wananchi wa maeneo mbalimbali Mkoani Mwanza, wamejitokeza kwa wingi kufanyiwa uchunguzi wa Masikio, baada ya Shirika la Starkey Hearing Foundation kutoka
nchini Marekani kutoa huduma hiyo Jijini Mkoani Mwanza bila malipo.
idadi kubwa ya wakazi wa Mkoa wa Mwanza wameitikia wito wa kufanyiwa uchunguzi kutokana na wengi wao kuathiriwa na matatizo mbalimbali ya Masikio.
Serikali alieleza kuwa lengo la kutoa huduma hiyo katika Mkoa wa Mwanza ni kwa ajili ya kuwasaidia
watu wenye matatizo ya masikio hususani viziwi, sanjari na wale ambao masikio yao yanakuwa na uchafu wa muda mrefu unao wasababishia
kutosikia kama vile usahaa na kuziba kwa ngoma ya sikio.
Alisema watu
wanaokutwa na matatizo kama hayao, husafishwa na kupatiwa dawa maalumu zitakazo wasaidia kusikia vizuri kama kawaida .
“Watu wanaogundulika kuwa na tatizo la kutosikia, hasa
kwa viziwi, tuna kifaa maalumu (Hearing Aids) ambacho hutumia betre kwa muda wa
miaka 5, tunawapatia kifaa hicho kila mmoja cha kwake ili kuweza kuwasaidia kusikia”.Alisema Serikali.
Alifafanua
kwamba, kifaa hicho kitawafanya waweze
kusikia kama awali, ikiwa ni pamoja na kuongea na simu, kusikiliza muziki na mada zinazo tolewa darasani na hata katika shughuli mbalimbali za kijamii
wanazo zifanya. Huduma hiyo ilianza kutolewa Jijini Mwanza tangu juzi Ijumaa Septemba 19 katika Shule ya Msingi Nyanza na inatarajiwa kufikia tamati leo Septemba 21.
Kwa upande
wake Mwalimu wa shule ya viziwi na mvalishaji wa vifaa vya usikivu kutoka
Arusha Raphaeli Lukumai, alisema kuwa huduma hiyo inatolewa katika Mikoa mbalimbali
ambapo kwa sasa wapo Kanda ya Ziwa ambapo tayari wananchi wanaosumbuliwa na matatizo ya kusikia katika Wilaya za Musoma na Bunda Mkoani Mara, wamekwisha nufaika na huduma hiyo
Raphaeli
alisema kuwa pamoja na kutoa huduma hiyo maeneo mbalimbali, bado wanakumbana na changamoto nyingi, ikiwa ni
pamoja na baadhi ya watu kuwa waoga
pindi wanapochukuliwa vipimo, baadhi kutokuwa na ngoma ya sikio kutokana kuchokonolewa mara kwa mara kipindi wanapokua wanatoa
uchafu sikioni.
Rachel Daniel ambaye ni mmoja wa wagonjwa wa kutosikia jijini Mwanza, alieleza
kuwa amefurahi kupata huduma hiyo, kutokana na kuwa awali alishindwa kupata huduma hiyo muhimu kutokana
na kutokuwa na fedha kwa ajili ya kulipia gharama kwa ajili ya matibabu ama kununua
kifaa hicho kinachompa mtu asie sikia uwezo wa kusikia.
Katika kuhitimisha ufafanuzi wake, Wilfred Serikali ambae ni Mratibu wa Chama cha Kuhudumia Viziwi Tanzania ( Starkey Hearing Foundation) alieleza
kwamba chama hicho kinafanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia wizara ya Afya na Ustawi wa jamii na wizara ya
elimu na mafunzo ya ufundi, ambapo kambi
hiyo ya kutoa huduma kwa watu wenye matatizo ilianzishwaa tangu mwaka 2008 hapa nchini.
Na Prisca Japhes.
Na Prisca Japhes.
No comments: